Wednesday, July 19, 2017

ALAMA 15 ZA ROHO MTAKATIFU

ALAMA ZA ROHO MTAKATIFU

Kutokana na utendaji na madhihirisho ya kazi  na huduma za Roho Mtakatifu, imempendeza Baba kwamba Roho Mtakatifu awe na alama zinazo mwakilisha.Alama hizi tofauti zinaweka wazi asili,tabia na kazi za Roho,kama vile ilivyo kwa alama za Yesu Kristo ,Mwana wa Mungu.



Alama 15 Za Roho  Mtakatifu.

  1. ALAMA YA MAJI

 Alama ya hii ya maji  inapotumiwa kwa Roho Mtakatifu inawakilisha juu ya utoaji wake wa uzima unaotiririka unaoleta uahi mpya,pia inawakilisha kazi yake ya kuosha na kusafisha na kuzaa matunda. Maji ni alama ya Roho Mtakatifu kwa maana  ya kuwa mito itatoka ndani yetu baaad ya kubatizwa katika Roho Mtakatifu.(Yohana 7:38,39, 4:4, Zaburi 72:6, 87:7, Isaya 44:3, Kutoka 17:6, I Kor.10:4)

2.ALAMA YA MOTO
Alama hii ya moto inatumika kuonyesha utakatifu wa Mungu ambapo Roho Mtakatifu anahusika kuhukumu na kusafisha na kutakasa kama moto.Roho anashuhudia , kuhakikisha na kuhukumu dhambi. Ubatizo wa Roho huambatana na moto wa kiroho .(Mathayo 3:11, Matendo 2:3, Isaya  4:4, Kutoka 19:18, Malaki 3:2-3, Waebrania 12:29)

 3.ALAMA YA UPEPO AU PUMZI.
Alama hii inaashiria utoaji wa uzima wa   pumzi ya Mungu katika nguvu yake ya kutoa uhai mpya.Hii inasisitiza ukweli kwamba Roho Mtakatifu ni Nafsi isiyo onekana lakini bado athari za utendaji wake zinaweza kuonekana. ( Matendo 2:2, Yohana 3:8;Ezekieli 37:9-10 ,Isaya 40:7)

4. ALAMA YA UMANDE
 Alama hii inaashiria kazi ya Roho Mtakatifu  ya kulifariji na kulichangamsha kanisa. kulifanya liwe hai wakati wote.( Zaburi 133:1-3, Hosea 14:5)

5.ALAMA YA MAFUTA
Alama hii ya Roho Mtakatifu inazungumza juu ya mambo haya yafuatayo;kuwekwa wakfu na Uwezo wa Kimungu wa Roho Mtakatifu,Neema ya upako,Uwepo wake wa Uponyaji, na Mwangazio wa mafundisho yake.Ni Roho ambaye huwatia mafuta(kuwateua na Kuwasmika) waamini wa kanisa kwaajili ya kazi za kitumishi. (Luke  4:18, Matendo 10:38, 1 Yohana  2:20,27, Zaburi 23:5

6. ALAMA YA NJIWA.
Alama  ya  njiwa inatumika  kuwakilisha usafi,uzuri,upole, Amani na asili na tabia za Roho Mtakatifu kwa Ujumla.(Mathayo 3:16, Luka 3:22,Mwanzo 1:2, Mathayo 10:16)

 7.ALAMA YA MHURI.
Mhuri ni alama ya umuhimu ya kuonyesha umiliki,na usalama.Alama  hii inasisitiza juu ya kazi ya Roho Mtakatifu ya kututhibitisha mbele za Mungu kwamba Yeye Anatumiliki,tu wake,na ana mamlaka juu yetu na usalama wetu upo kwake. (Efeso 1:13,4:30, 2 Kor. 1:22, 2 Timotheo 2:19)

8.ALAMA YA SAUTI NDOGO YA UTULIVU.
Roho  ni sauti ya Mungu ndani ya mtu inayoleta ufunuo wa mapenzi ya Mungu kwake.Mwanzo 3:8, 2 Wafalme 19:11-13

9.ALAMA YA KIDOLE CHA MUNGU.
Roho ndiye anayeonyeshea kidole cha kumshitaki mwenye dhambi ,kumfanya avutwe na kukujisikia mwenye hatia hata kumpelekea ampokee Yesu Kristo kama mtetezi wake(wakili wake) Luka 11:20, Mathayo 12:28

10.ALAMA YA MALIMBUKO.
Malimbuko ilikuwa ni alama ya mavuno kamili yanayokuja, Alama hii inaonyesha vile kazi ya awali ya Roho Mtakatifu ya kuifanya upya roho ya mwamini(kuzaliwa mara ya pili) inapelekea kwenye wokovu kamili na kutukuzwa kwa mwamini mbele za Mungu. Warumi 8:23

11.ALAMA YA DHAMANA
Dhamana Ni malipo ya mwanzo yanayo ashiria malipo kamili yatakayafuatia.Alama hii  ni kuonyesha vile Kazi ya Roho katika wokovu wetu ni sehemu ya mwanzo ya kazi kamili na kuu ya ukombozi utakao kuja.Alama hii inafanana na ile ya malimbuko. (Efeso 1:13-14, 1Kor. 1:22)

12.ALAMA YA VAZI AU KUVIKWA
Alama hii ya kuvikwa inamaanisha kumvaa Roho Mtakatifu,yaani Roho kuwa juu ya mtu.Ubatizo wa Roho Mtakatifu ni kama kuvaa vazi la kiuungu kutoka juu.Ni vazi la mwamini kwaajili ya huduma mbele za Bwana. (Luka 24:9,Waamuzi 6:34, Isaya 61:10,)

13.ALAMA YA NAMBA SABA.
Namba saba inatumika kuhusisha ufunuo wa Roho Mtakatifu,Ni alama ya ukamilifu,kukamilika ,na kamili,Inawakilisha ukamilifu wa utendaji wa Roho katka ulimwengu. Taa saba,Macho saba,pembe saba,Roho saba . (Ufunuo 1:3-4,4:5,5:6)

  14.ALAMA YA NURU
Roho ni Nuru.Taa saba hizi ni alama za Mwangazio,ufunuo,na uvivio wa Roho Mtakatifu. Macho  saba , Macho saba ni alama ya kuona, ufahamu,kupambanua,Akili, Hii ni ishara wa Roho wa kujua yote, ukamilifu wa kuona na kufahamu yote.( Ufunuo 1:3-4,4:5,5:6)Tunapozaliwa upya nuru huja ndani ya mtu wa ndani kwasababu Roho wa Mungu huingia ( 2 Wakorintho 4:6 Zekaria  3:9,4:10)

15.ALAMA YA NGUVU AU UWEZO.
Pembe Saba ni alama ya nguvu na ulinzi, zinawakilisha uwezo wote,Roho ana nguvu zote. (Ufunuo 5:6). Roho Mtakatifu ni alama ya nguvu na uwezo utakao juu ndani ya mwamini. ( Matendo 1:8, Luka  34:49)


Pastor & Teacher
Meinrald Anthony Mtitu.

No comments:

Post a Comment

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...