Sunday, September 24, 2017

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI



Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu

Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtoleaje ?Kila mmoja anaweza kujifunza kutoa,lakini pia inahitaji nidhamu kuwa mtoaji.Hapa ni kanuni 21 za vile tunaweza kumtolea Mungu na hivi ndivyo utoaji wetu unavyopaswa kuwa.



1. TOA KWA UPENDO:

Upendo unapasa kuwa ndiyo kisababisho kikuu nyuma ya kutoa kwetu. Upendo unapaswa kuwa ndio Nia nyuma ya kutoa kwetu.Sio lazima tuoe kwasababu fulani,upendo hautafuti sababu ya kufaidika katika kutoa huko.Tunapotoa kwa upendo si lazima tutoe ili sisi kufaidika. Ukitaka kutoa basi toa bila uchoyo.

“ Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia” Waebrania 6:10


2. TOA KWA KUABUDU ;

Kuabudu ni tendo lolote lile linalo mpa Mungu utukufu, (I Wakoritho 10:31).Kutoa ni sehemu ya Ibada. Askofu David Oyedepo anashauri hivi ,“Toa kama sehemu yako ya Ibada kwa Mungu. Tunatoa kama kuabudu hivyo hatutoi ili kupokea,lakini uaminifu wake Mungu huturudishia Baraka kwetu.”

Hatutoi kama kucheza kamali,Sadaka sio toa na kupokea. “cash and carry”.Ikiwa unatoa tu kwaajili ya kupokea utaaishi kuvunjika moyo na hutaziona Baraka.Toa kama sehemu ya kuabudu.

Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu, Tetemekeni mbele zake, nchi yote.” Zaburi 96:8-9

3. TOA MARA KWA MARA

Kutoa iwe ni sehemu ya maisha yako,hivyo toa mara kwa mara,kila wiki,kila mwezi n.k.Kutoa ni tabia unayoweza kujifunza ni matokeo ya kitendo unachokifanya mara kwa mara.Kadiri tunavyopata nafasi au fursa tuzitumie kuwatendea mema watu wengine.Tafuta fursa za kutoa.Ukizitafuta zitaanza kujitokeza.

“Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho. Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.”-Wagalatia 6:9-10

4. TOA KWA KUMHESHIMU MUNGU:

Kutoa ni ni njia moja wapo ya kumheshimu Mungu.Ni kuonyesha heshima mbele zako,unatambua yeye ni nani na nini anafanya katika maisha yako. “Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.” Mithali 3:9-10,

5. TOA KWA KUKUSUDIA

Toa vile unavyokusudia moyoni mwako au vile unavyoguswa na Kusukumwa.Usitoe kiholela bila kusudi.Huwezi kutoa kwa kila jambo tu,tafuta kusudi la kutoa kwako. Unataka kutoa kwaajili ya kusudi gani?,jambo gani,?eneo gani?,kwaajili ya nini? Tunatoa kwa uangalifu na kwa kupanga katika maombi.Panga kabla kusudi kabla ya kutoa.Panda mbegu yako katika udongo mzuri,usitupe tu mbegu zako hovyo.

“Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.” 2Wakorintho 9:7


6. TOA KWA MOYO WA FURAHA

Kutoa kunapaswa kuwa ni tendo la furaha.Usitoe kwa moyo wa huzuni bali kwa kufuraha.Hisia zako katika kutoa ziwe chanya.Kutoa hakupaswi kuwa na hisia ya maumivu au majuto kwa baada ya kutoa. “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu” 2 Wakoritho.9:7


7. TOA KWA UKARIMU

Ukarimu ni kwa kujali wengine. Ukarimu ni hali ya kujali mahitaji ya watu wengine.Mtu mkarimu anatoa kwa mguso wa ndani,(2 Wakorintho.9:6,13;).Unapotoa kwa ukarimu ni kama unatawanywa,lakini ndivyo unavyoongezewa.” . MTIHALI 11 :24-25
TOA KWA NEEMA YAKE MUNGU.

Utoaji unapaswa kuwa ni matokeo ya kazi ya neema yake Mungu katika maisha yetu,kunaanza kwanza kujitoa kwa maisha yetu yote kwake ,na utoaji ni kama kujazilizia kujitoa kwetu. (2 Kor. 8:1-2,6-7, 9:9-11

2. TOA KWA IMANI

Toa kwa imani ukijua Yeye ameahidi kutupa mahitaji yetu yote,hatutapungukiwa kwa kutoa kwetu,hatutakuwa wahitaji kwasababu tumetoa ( 2 Wakor. 9:7. Wafili 4:19) WAEBRANIA 11:6

3. TOA KI- KIBINAFSI.

Unapotoa toa kama wewe binafsi.Linapokuja suala na utoaji Sio lazima tusuburi utoaji wa pamoja wa kundi au watu wengine.Kutoa kwenye tija katika ufalme wa Mungu ni kule ambako kunasukumwa toka ndani ya kibinafsi.Sio lazima tusubiri mtangazo ndipo tutoe.

( I Wakoritho 16:2)

4. TOA KWA MFUMO

Katika utoaji unayo nafasi ya kujiwekea mfumo wako ambao utautumia katika kumtolea Mungu.Hivyo toa kwa mfumo uliochagua na kujiwekea.Unaweza kuwa na mfumo wa kutenga na weka akiba ya kiasi ambacho unataka kutoa kwaajili ya Bwana ili kisitumike kwaajili ya kusudi jingine.( I Kor 16:2)

5. TOA KWA KADIRI NA UWIANO:

Toa kwa kadiri na uwiano wa ulivyofanikishwa.Katika Agano Jipya tunatoa zaidi kwa kufuata kanuni ya Neema na hiari,kwa kukusudia na kwa kadiri ya vile ulivyofanikishwa.Kadiri unavyokuwa na vingi zaidi toa zaidi.

2 KOR.8:14 Kumbu 16:17, Matendo 11:28-30 I Kor. 16:2,2 Kor:8:3,12, Marko 12:41-44,


6. TOA KUTOKA KATIKA UWINGI.

Toa toka katika uwingi wa vile ulivyo navyo..Kadiri unavyo kuwa na vingi ndivyo unavyotarajiwa kutoa zaidi.

Kumb 28:47,2 Wakor. 9:7


7. TOA KWA HIARI:

Toa kwa hiari yako na kutaka kwako mwenyewe.Maamuzi ya kutoa yaye ni ya kwako mwenyewe,toa kwa kupenda toka ndani.Toa kwa utashi wako mwenyewe ukijua unachofanya,maamuzi ya kutoa yatoke ndani yako.Usitoe kwa msisimko,kwa kufauta mkumbo au kuiga. Toa kwa hiari.( I Nyakati 29:6 Kutoka 25 :2 2 Kor.9:7)

8. TOA KWA UHURU

Toa kwa uhuru bila ya kushinikizwa kutoka nje, Usitoe kwa kufanyiwa hila,kulazimishwa,kutishiwa.

Mtihali 11:24 Warumi 11:35

9. TOA KWA UNYENYEKEVU:

Kutoa kunaanza ni hali nzuri ya ndani yako.Toa kwa unyenyekevu si kwa majivuno,kiburi au kujionyesha.Kabla ya Mungu hajaangalia sadaka yako anakuangalia wewe. MIKA 6:8 MATH.6:2-4


10. TOA KWA NIA NJEMA.

Toa kwa nia njema na na sio kwa hila ,sio kwa sababu au agenda ya siri .Nia yako ya kutoa lazima iwe ni ukarimu,upendo,kumwabudu Mungu n.k.Kutoa kwa nia ya kupokea ni kama kucheza kamali.Mungu hachezi kamali.Ezekiel 33:31, Mathayo 6:33


11. TOA KWA KUWAJIBIKA

Toa kama wajibu wako kama Mkristo.Unapotoa unatimiza wajibu wako wa kiroho. Nehemia 10:34-39 Luka 16:1,2,10

12. TOA KWA KUJIKANA

Toa kwa kujikana nafsi, unabakiwa na kiasi gani baada ya kutoa ndiko kunaonyesha ulijikana kwa umbali gani. Kujitoa kwa kujikana,Daudi alikuwa na Mtazamo huu katika kutoa kwake)hatupaswi kumtolea Mungu wetu mabaki,au makombo,tumtolee kilicho bora na kizuri.Angalia karipio la Nabii Malaki.Mtume paulo anatutaka Kila mmoja wetu anahitaji atathimini upya utoaji wake.( 2 Wakoritho 2:8 Marko 12:41-44, Malaki 1:12-14 2 Samuel 24:24)

13. TOA KWA SIRI

Pale inavyowezekana toa kwa siri.Sio mara zote lazima watu wajue ulivyotoa.Unaweza toa kwa siri na Mungu akakubariki. kutoa kuwe ni kwa usiri pale inapowezekana.Kutoa si mashindano ,kila mtu anatoa kwa kadiri ya neema na alivyojaliwa.( Mithali 21:14, Mathayo 6:2-4)

14. TOA KWA KWA SHUKURANI :

Utoaji ni sehemu yako ya ibada ya shukurani kwa Mungu.Toa kama sehumu ya shukurani kwa Mungu kwa mambo mengi mno aliyekutendea.(I Nyakati 29:9, 2 Wakoritho 9:11)

15. TOA KWA UHURU

Toa kwa uhuru bila ya kushinikizwa kutoka nje, Usitoe kwa kufanyiwa hila,kulazimishwa,kutishiwa.

Mtihali 11:24 Warumi 11:35

16. TOA KWA UNYENYEKEVU:

Kutoa kunaanza ni hali nzuri ya ndani yako.Toa kwa unyenyekevu si kwa majivuno,kiburi au kujionyesha.Kabla ya Mungu hajaangalia sadaka yako anakuangalia wewe. MIKA 6:8 MATH.6:2-4

17. TOA KWA NIA NJEMA.

Toa kwa nia njema na na sio kwa hila ,sio kwa sababu au agenda ya siri .Nia yako ya kutoa lazima iwe ni ukarimu,upendo,kumwabudu Mungu n.k.Kutoa kwa nia ya kupokea ni kama kucheza kamali.Mungu hachezi kamali.Ezekiel 33:31, Mathayo 6:33

18. TOA KWA KUWAJIBIKA

Toa kama wajibu wako kama Mkristo.Unapotoa unatimiza wajibu wako wa kiroho. Nehemia 10:34-39 Luka 16:1,2,10

19. TOA KWA KUJIKANA

Toa kwa kujikana nafsi, unabakiwa na kiasi gani baada ya kutoa ndiko kunaonyesha ulijikana kwa umbali gani. Kujitoa kwa kujikana,Daudi alikuwa na Mtazamo huu katika kutoa kwake)hatupaswi kumtolea Mungu wetu mabaki,au makombo,tumtolee kilicho bora na kizuri.Angalia karipio la Nabii Malaki.Mtume paulo anatutaka Kila mmoja wetu anahitaji atathimini upya utoaji wake.( 2 Wakoritho 2:8 Marko 12:41-44, Malaki 1:12-14 2 Samuel 24:24)

20. TOA KWA SIRI

Pale inavyowezekana toa kwa siri.Sio mara zote lazima watu wajue ulivyotoa.Unaweza toa kwa siri na Mungu akakubariki. kutoa kuwe ni kwa usiri pale inapowezekana.Kutoa si mashindano ,kila mtu anatoa kwa kadiri ya neema na alivyojaliwa.( Mithali 21:14, Mathayo 6:2-4)

21. TOA KWA KWA SHUKURANI :

Utoaji ni sehemu yako ya ibada ya shukurani kwa Mungu.Toa kama sehumu ya shukurani kwa Mungu kwa mambo mengi mno aliyekutendea.(I Nyakati 29:9, 2 Wakoritho 9:11)

Mwalimu Meinrald Mtitu

Light of Hope Teaching Ministries.


Friday, September 15, 2017

TABIA KUMI ZA MTU MVIVU




TABIA KUMI (10)  ZA MTU MVIVU

1. HUPENDA SANA USINGIZI NA KULALA KWA MUDA MREFU.

MITHALI 19:15- Uvivu huleta usingizi mzito, naye mtu mzembe huona njaa.

Kulala ni jambo la kawaida na la muhimu kwa kila mwanadamu. Kwaajili ya afya njema ya mwili na akili tunahitaji wastani wa masaa 6-8 ya kulala.Hakuna tatizo katika kulala ,tatizo ni pale kulala kunapo tumika kama kichaka cha kujifichia na kukwepa kufanya kazi.

MITHALI 26:14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.

Mtu mvivu huona vigumu sana kukiacha kitanda chake. Anapenda sana kulala kupita mahitaji ya kawaida ya mwili wake. Watu wenye uvivu uliojificha ndani yao wakiugua kidogo au kujisikia vibaya kidogo basi kitanda kita wakoma siku hiyo ,hawatatoka kitandani.

MTIHALI 6:9-10 Ewe mvivu, utalala hata lini? utaamka lini kutoka katika usingizi wako? Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono upate usingizi!

Kuna uvivu uliojificha nyuma ya kupenda kulala sana kupita mahitaji ya kawaida ya mwili na akili.

MITHALI 20 :13

Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.


Wako watu wavivu wanaokesha usiku wanaangalia luninga kiasi kwamba asubuhi hawezi kuamka,mchana kutwa wanashinda wamelala. Hii ni tabia ya uvivu. Wako watu wavivu ambao wanapenda mno usingizi kiasi kwamba hata wakijitahidi kutega kengele ya saa (Alarm) iwaamshe bado hawawezi kuamka. Wako watu wanaochelewa mara kwa mara kazini, shuleni au kuwahi usafiri kwaajili ya safari n.k.sababu kubwa ni uvivu uliojificha katika kupenda usingizi.


2. HUWA MLEGEVU KATIKA KAZI NA KUUPOTEZA MUDA KWA MAMBO YASIYO NA TIJA.


MITHALI 18:9

Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu...


Tabia nyingine ya mtu mvivu ni kupoteza muda,hajali muda kabisa. Katika zama hizi za teknolojia moja ya vitu vinavyo poteza muda ni pamoja matumizi ya mitandao ya kijamii kupitia simu za kisasa za “ Smart phone”, Michezo ya kwenye simu na komputya, vipindi vya televisheni hasa vile vya maigizo na filamu.Eneo jingine ni lile la kuwasiliana kwa simu maarufu kama ku-chat.

Kwa kuwa watu wengi walio wavivu hawana nidhamu binafsi ni rahisi sana kutekwa na kutumia muda wao mwingi sana katika maeneo hayo tena hata wakiwa kazini.

Kutumia masaa mengi kawa mambo yasiyo na tija sio tatizo kwa mtu aliye na uvivu uliojificha,haoni ni tatizo lolote kuwa katika makundi ya mitandao ya kijamii na kutumia muda wake wote huko.Hata kama ni makundi ya kujadili Biblia na mambo mengine ya manufaa, haingii akili kuona mtu yupo online na akijadiliana na kubisha kuhusu Biblia kwa masaa sita! Hivi huna mambo mengine ya kufanya?

MITHALI 14:23 Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida, bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.
Mtu mvivu utamwona yupo kwenye makundi karibia kumi ya facebook na whatsApp ,bado yupo kwenye mitandao ya Instragram,Telegram, Jamii Forum na mingineyo, na kila kundi kuna mada fulani inaendelea na anataka ashiriki kuchangia.Atafanya kazi saa ngapi?atafikiri saa ngapi?

Wavivu wengine wapo ofisini utaona wakati wote wapo kwenye mitandao,unafanya kazi saa ngapi? Huo ni ulegevu na uvivu! Kuna vitu vya muhimu zaidi katika maisha zaidi ya kuwa muda wote kwenye facebook ,Instragram na Twitter.

Kuna watu ukiwaachia kazi ya kufanya hawezi kuifanya kazi na kuikamilisha kwa wakati kwasababu muda wao wote wanaupoteza kuzungumza,kupiga stori,na mazungumzo yenyewe ni yale ya upuuzi tu.Wengine ni kupoteza muda wote kwenye simu,watapigia watu simu hata kama hawa jambo lolote la maana kwasababu tu amejiunga na kifurushi cha bei nafuu na ana muda hewani wa kutosha.Huu nao ni uvivu.



3. HUACHA MAMBO YANA HARIBIKA BILA KUCHUKUA HATUA.

MITHALI 24:30-31

Nilipita karibu na shamba la mtu mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili, miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.




Mtu mvivu hawawezi kutengeneza vitu vinavyo haribika .Watu wavivu wanatabia ya kuacha mambo yanaharibika bila ya kuchukua hatua hata kama jambo husika lipo katika uwezo wao kulirekebisha.Wana acha hata nyumba zao zina haribika na kuvuja bila kufanya marekebisho kwa wakati.Mambo madogo ambayo wangeweza kuyashughulikia yataachwa hivyo kwa muda mrefu.

Nguo inaweza kubaki imechanika au kutatuka mahali bila ya kushonwa kwa muda mrefu tu kitu ambacho ni kidogo sana.Wengine kurudishia kishikizo tu kwenye shati inaweza kuchukua miezi na anaendelea kulivaa!Wengine ni viatu vilivyotatuka vitaendelea kuvaliwa bila marekebisho.

MHUBIRI 10:18

Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.


Kushindwa kufanya marekebisho na matengenezo madogo madogo tu ni dalili ya uvivu uliojificha. Hii inaendana na tabia nyingine ya kuahirisha mambo tutayoiangalia hapo mbele.



4. HUJAA UDHURU WA KUAHIRISHA MAMBO BILA SABABU ZA MUHIMU.

MITHALI 22:13

Mvivu husema, ‘‘Kuna simba nje!’’ au, ‘‘Nitauawa huko njiani.


Watu wavivu hutafuta sababu za kipuuzi za kutoka kufanya kazi. Wamejaa udhuru na “visababu” vya kuwepa kufanya kazi.Nyuma ya sababu zao kuna uvivu “ uliojificha”.Wakati wote wanatafuta udhuru wa kipuuzi wa kutofanya kazi na hawaukosi!


MITHALI 26:13

Mvivu husema, ‘‘Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”



Ukimpa kazi mtu mvivu hatakosa sababu ya kutoikamilisha. Kwa kila sababu unayompa ya kufanya kazi,yeye atakupa sababu mbili ya kwanini asifanye kazi hiyo. Mtu mvivu si wakuachiwa kufanya jambo,mwachie mtu mvivu na hakuna kitu kitafanyika.

Kauri mbiu ya watu wavivu ni “kamwe usifanye leo lile unaloweza kuliacha mpaka kesho”. Watu wavivu ni wepesi kughahiri jambo na kuahirisha jambo tena bila sababu.

Mtu mvivu huwa haheshimu na kufuata ratiba aliojiwekea mwenyewe. Kuna ushauri wa hekima unasema “Usiache lifanyike kesho lile unaloweza kulifanya leo”.Ingawa ,watu wavivu wao wanasema“Kwanini ufanye leo lile unalo weza kufanya kesho?”


MITHALI 20:4

Mvivu halimi kwa majira, kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati cho chote.


Mtu mvivu anaweza kujitetea kuna joto sana au kuna baridi sana , ingawa wengine wote wanafanya kazi katika hali hiyo hiyo ya hewa.Anaweza akaacha kufanya kazi kwa hofu ya kuumia,ingawa uwezekano wa kuumia ni mdogo sana au haupo kabisa.

MITHALI 26:16

Mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wajibuo kwa busara.


Katika Mathayo 25.kuna mfano wa Talanta,Bwana aliyesafiri kwenda nchi ya mbali aliwapa watumishi wake talanta (fedha za wakati huo) ili wazizalishe mpaka atakapo rudi.Wawili walifanya fanya bidii na kuzalisha,lakini mmoja hakufanya kitu alifukia talanta aliyopewa.Na Bwana wake aliporudi alitoa sababu za kipuuzi kwanini hakuzalisha fedha aliyoachiwa hebu sikia sababu zake za kipuuzi .

MATHAYO 25:24-29:

“Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba wewe ni mtu mgumu, unayevuna mahali usipopanda na kukusanya mahali usipotawanya mbegu. Kwa hiyo niliogopa, nikaenda, nikaificha talanta yako ardhini. Tazama, hii hapa ile iliyo mali yako.’

“Bwana wake akajibu, ‘Wewe mtumishi mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna mahali nisipopanda na kukusanya mahali nisipotawanya mbegu. Vema basi, ingekupasa kuweka fedha yangu kwa watoa riba, nirudipo, nichukue ile iliyo yangu na faida yake?


‘‘ ‘Basi mnyang'anyeni hiyo talanta mkampe yule mwenye talanta kumi.’Kwa maana kila mtu mwenye kitu ataongezewa, naye atakuwa navyo tele. Lakini kwa mtu yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa.

Sababu anazozitoa ni za kipuuzi,nyuma ya sababu hizi zote ni uvivu tu ndio ulikuwa tatizo lake.Huyu mtumishi mvivu hakujua kuwa ukiweka fedha aridhini haiwezi kuota. Alipaswa kujaribu hata kuweka benki,angepata riba kuliko kuto fanya chochote.Na Yule Bwana alimwita ni mwovu na mvivu.


5. HUSUBIRI MPAKA MAZINGIRA YAWE SAHIHI NDIPO AFANYA KITU.



MITHALI 19:24

Mtu mvivu huuzamisha mkono wake kwenye sahani, lakini hawezi hata kuurudisha kwenye kinywa chake!


Watu wavivu hawana msukumo na motisha ya kufanya mambo. Watasubiri mpaka mazingira yote yawe sahihi ,yawe vizuri ndipo utawaona wanashughulika .Baadhi ya watu wavivu hawana hamasa kabisa na kazi,hawana tamaa ya kufanya mambo makuu ndani yao.

Kuna watu waliozaliwa au kukulia katika mazingira ambayo ni rahisi kuwafanya kuwa wavivu.Wananunuliwa kila kitu,hawajajifunza kuzalisha chochote kwa nguvu zao,hawawezi kuchuma wao wenyewe. Wamezoea na kujifunza kusubiri mtu mmoja awape mkononi !

MITHALI 26:15 Mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye hushindwa kuurudisha tena kinywani mwake.


Ni vizuri watoto wafundishwe kazi wakiwa bado wadogo wasifanyiwe kila kitu! Wapo watoto wamekuwa hawajui hatakufua soksi zao tu! Kila kitu walikuwa wanafanyiwa.



6. HUTUMIA VIBAYA KILE ALICHONACHO.


MITHALI 12:27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.

Mtu huvivu atapanya na kufuja kile alichonacho.Mtu mvivu hawezi hata kukitunza kile alichonacho.Uvivu wake utamfanya hata kile alicho nacho kiharibike kabisa na kuchakaa .

MITHALI 24:30-31

Nilipita karibu na shamba la mtu mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili, miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.


Kuna baadhi ya vitu haviwafahi kabisa watu wavivu, hasa vile vinavyohitaji usimamizi na uangalizi wa karibu na marekebisho ya mara kwa mara. Ukiwapa hesabu ni hasara tupu. Kuna watu wanakaa na chakula mpaka kinaharibika kwaajili ya uvivu wa kukipika tu.

Kuna watu wanaacha nguo kwenye maji mpaka zinaharibika kwaajili ya uvivu wa kuzifua tu.Kuna watu wanaacha shamba lina haribika kwasababu ya uvivu wa kulipalilia kwa wakati.

MITHALI 18:9 Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu.

Watu wavivu ni waharibifu wa vitu,wape kazi yako wataiharibu tu.

7. HUTAMANI MAMBO MENGI LAKINI HAWEZI KUZALISHA.

MITHALI 21:25-26 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi. Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.

Watu wavivu wanazao shauku na matamanio lakini hawezi kuzitimiza. Hata wakiwa na ndoto haziwezi kutimia.Wavivu wengi wanaota ndoto za mchana wakiwaza kuwa na mambo makubwa lakini hayatakamilika maishani mwao.

MITHALI 26:15 Mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye hushindwa kuurudisha tena kinywani mwake.

MITHALI 19:24

Mtu mvivu huuzamisha mkono wake kwenye sahani, lakini hawezi hata kuurudisha kwenyekinywa chake!

8. HAKUBALI KUTAMBUA KWAMBA YEYE NI MVIVU

MITHALI 26:16

Mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wajibuo kwa busara.

Watu wavivu huwa wakubali kwamba wao ni wavivu,wana hekima machoni pa wenyewe.Hata mtu mvivu hapendi na anachukia akiambiwa wewe ni mvivu. Watu wavivu si waanzishaji wa mambo ,watasubiri wengine waanzishe na wao hatimaye wahamasike.Watu wavivu hatawakianza jambo huwa hawalimalizi,wana weka mambo mengi viporo.Wanaweza kuwa na mipango mingi lakini yote haikamiliki.

Watu wavivu si waanzilishaji wa mambo na hawamalizi yale wanayoanza. Wana maisha yalivugurukika yasiyo na mpangilio.Maisha ya watu wavivu hayana mpangilio,wana maisha yaliyo vurugika.



9. HUPENDA KUWA TEGEMEZI NA KULEMEA WATU WENGINE.


2 WATHESALONIKE 3:8

wala hatukula chakula cha mtu ye yote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu ye yote miongoni mwenu.


Watu wavivu wanapenda vitu vya bure ,wanakwepa kugharimika. Wengi wanatabia za kuwalemea watu wengine na kugeuka mzigo.Watu watakusaidia lakini uje pia watu watakuchoka.Wako watu wana tabia ya kuomba omba vocha za simu,nauli na vitu kama hivyo mpaka watu wanawachoka.Kuna msemo unasema; “hakuna chakula cha bure,kile unachokiona ni cha bure ujue kuna mtu mwingine amekilipia gharama.”

I Wathesalonike 4:11-12

Jitahidini kuishi maisha ya utulivu, kila mtu akijishughulisha na mambo yake mwenyewe na kufanya kazi kwa mikono yake, kama vile tulivyowaagiza, ili maisha yenu ya kila siku yajipatie heshima kutoka kwa watu walio nje, ili msimtegemee mtu ye yote.


10. HUFANYA KAZI ZAKE KWA ULEGEVU NA UZITO.
MITHALI 18:9

Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu...


Mtu mvuvi hufanya kazi kwa uzito,kazi ya kuchukua muda mfupi na siku chache kwa mtu mvivu itachukua muda mrefu na siku nyingi bila sababu za msingi.Mtu mvivu ni goigoi,anajivuta sana katika kufanya shughuli zake.



Mwalimu M.A.MTITU




Wednesday, September 13, 2017

KUBADILISHWA KUPITIA MATESO



KUBADILISHWA KUPITIA MATESO 

Tunapokutana na nguvu za Mungu tukiwa katika mateso tunakuwa kama Ayubu.Maswali yetu yote kwa Mungu, malalamiko yetu yote yanayeyuka na tunaishia kuanguka mbele zake kwa hofu na kumwabudu.Tunakuwa hatuna tena cha kuzungumza mbele zake.
AYUBU 42:1-6

Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema. Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika. Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua. Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie. Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. Kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu, na kutubu Katika mavumbi na majivu.

Baada ya Ayubu kumtaka sana Mungu ajitokeze na amjibu kwanini anamtesa,hatimaye katika sura ya 38-41 Mungua najitokeza kupitia Upepo wa Kisurisuri na kumjibu Ayubu kwa kumuuliza maswali mbalimbali.Hatimaye sasa katika Sura ya 42 Ayubu anasalimu amri anamwelewa Mungu na hana swali tena kuhusu kwanini anateseka.Kile kitendo cha kukutana na uwepo wa Mungu kinabadilisha,mtazamo wake unabadilika,maswali yake yanaisha na kukoma.


Ayubu atanapata uzoefu mpya na anahitimisha kwa kile alichojifunza pale Mungu alipomtokea. Mungu halimjibu Ayubu kwa mahojiano na sio kwa kujibu maswali yake.Mungu alijibu kwa kujitokeza tu kwa uwepo wake.Hilo tu lilitosha kumbadilisha Ayubu.

Nafikiri wakati mwingine tukiwa katika vipindi vya mateso kama Ayubu tunachohitaji zaidi ni uwepo wa Mungu tu ,huuo utamaliza maswali yetu yote.Na kubadilisha matazamo wetu kuhusu mateso tunayoyapitia.

Baada ya Mungu kutokea na Kuhojiana na Ayubu tunanona hata alipopata nafasi ya kuzungumza ,alizungumza kama mtu aliyebadilika kabisa na aliyenyenyekea sana.Hakuendelea tena kuwa na madai ya majibu toka kwa Mungu.Hakuendelea tena kushikiria msimamo wake na kusisitiza kuwa yeye ni mwenye haki hivyo hakusatahili hayo mateso.

Baada ya hapo Ayubu alikuwa kimya.Baada ya maneno yote katika sura za nyuma ,hakuna tena maneno yanayorekodiwa kutoka kwenye kinywa cha Ayubu. Kumwona Mungu,na kuelewa Nguvu za Mungu kulibadilisha kabisa mtazamo wa Ayubu.Aliifanya upya hofu yake ya Mungu na ilikuwa ni hofu nzuri.

Mambo Makuu Matano Yakujifunza Katika Vipindi Vya Mateso

Masomo haya ni ya muhimu,hasa kama kama utakuwa kwenye msimu wa maumivu na kuteseka.Kile Ayubu aligundua kupitia mateso yake miaka mingi iliyopita hata leo kinawapa watu nuru ya ukweli ambao bado haujapoteza nguvu yake.


1. Mungu anaweza kutenda mambo yote.

AYUBU 42;1-2

Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema. Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote.

Ayubu alijifunza juu ya uwezo na ukuu na enzi ya Mungu.Alikiri kwamba hakika Mungu anaweza kutenda mambo yote.Yeye anatawala juu ya vyote.Hili ni somo kubwa sana la kujifunza.Baada ya kupitia katika mateso Imani ya Ayubu ili kuwa imetakaswa na imeimrika zaidi.Aliaamushwa na kuwa na ufahamu Mpya wa Kina kuhusu Mungu na uwepo na ukuu wake.Sasa imani yake imepita katika moto na amekuwa na kumjua Mungu kwa karibu zaidi.

Kumbe katika mateso tunapata nafasi ya kumjua Mungu kwa upya. Kuna kupata ufunuo mpya kupitia mateso ambao usingeweza kuupata kwa njia yeyote ile.


2. Makusudi yake Mungu hayawezi kuzuilika

AYUBU 42 : 2b Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika. 

Jambo jingine ambalo Ayubu alijifunza katika mapito yake ni kuhusu makusudi ya Mungu. Aliyefahamu makusudi ya Mungu na akaukubali ukweli kwamba makusudi ya Mungu hayawezi kuzuilika. Ayubu alijifunza somo kuhusu njia za Mungu kwamba Mungu anakwenda kufanya kile anachoenda kufanya.

Mungu hutuamsha tuujue ukweli kwamba Yeye ni Mungu wa makusudi. Mungu anayo makusudi na maisha yetu na anapokusudia kufanya jambo haiwezekani kwa chochote kile kulizuia hilo kusudi lake.Wakati mwingine ni kupitia hayo mateso tunayatambua makusudi ya Mungu na kujisalimisha kwake.



3. Ufahamu wetu ni mdogo kuelewa Maarifa ya Mungu ya kuruhusu Mateso kwetu. 


Ayubu 42:3

Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua. 

Baada ya kuziona njia za Mungu katika Ukuu na enzi yake Ayubu alikiri kwamba ufahamu ulikuwa ni mdogo sana kuelewa kwanini anateseka. Alitambua kwamba hata kama Mungu angemwelezea kila kitu anachofanya na kumchambulia kimoja kimoja bado asingeweza kuzielewa njia za Mungu kwani ni kuu sana kwa akili yake kuelewa. ( Isaya 55: 8-9). Alijifunza kwamba kuna wakati katika mahusiano na Mungu huitaji kujua kwanini; unahitaji kuwa mtii tu.


4. Maarifa ya Mungu ni makuu sana na ya kushangaza sana.

Ayubu 42:5

Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. 

Mahusiano ya Ayubu na Mungu yalikuja kuwa ni ya kina na ya karibu kwasababu ya yale aliyopitia.Ni kweli kuanzia mwanzo hata kabla ya kupitia mateso alikuwa ni mtumishi mcha Mungu na mwaminifu,lakini sasa anazunguza juu ya ufunuo binafsi alioupata wa kukutana na Mungu uso kwa uso. Kukutana kwake na Mungu kulifanya kila kitu katika maisha yake kubadilika.

Kupitia mateso uhusiano wetu na Mungu unakuwa ni wakaribu na halisi .Hakuna wakati tunakutana na uwepo wa Mungu kwa karibu kama wakati wa mateso. Ni katika nyakati kama hizo ni rahisi zaidi kupata ufunuo wa Kibinafsi kuhusu Mungu.

Wakati Shetani anataka kutumia maumivu yako kukufanya ukwazike na kukosana na Mungu;Mungu anataka kutumia maumivu yako kukuvuta kwake ili aweze kuleta badiliko ndani yako.Kitu kile kile ambacho Shetani anataka kuyatumia mateso kukufanya akuvute mbali na Mungu ,Mungu atatumia mateso haya hayo kufanya wewe kumjua Yeye kwa ukaribu zaidi kuliko Mwanzo.

5. Mateso hutufanya kupondeka na kujishusha mbele za Mungu.

AYUBU 42:6

Kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu, na kutubu Katika mavumbi na majivu. 

Mara nyingi Mungu alipojifunua kwa watu katika Biblia ,huu ulikuwa ndio mwitikio wa kawaida.Ayubu alipotokea na Mungu katika mateso yake alipondeka na kujishusha mbele zake.Kuna hali kuu sana ya kujiona hastahili na mwenye upungufu. Ili hali ya Ayubu aliyokuwa ameing’an’gania ya kujiona ni mwenye haki na hastahili kuteseka ilikwisha.

Mateso yanatunyenyekeza na kutufanya tumtegemee Mungu.

Ayubu alifanya toba kwa maneno yake na mwitikio wake mbaya aliouonyesha katika kipindi chote cha kujaribiwa katika mateso.Tunamwona Ayubu Mpya ambaye amenyenyekea na kupondeka kabisa. Ambaye mbali na nje ya Mungu anatambua kwamba ana haki ya kujihesabia,anayetambua udhaifu wake, upungufu wake, kutokuwa na umuhimu na utupu wake .

Kwasababu ya kutakaswa kwa moto wa mateso Ayubu sasa ametoka akiwa anaweza kutembea katika unyenyekevu mbele za Mungu na kumtegemea Mungu katika maisha yake yote.

Watu wengine Majaribu yana washinda, lakini wengine yana waimarisha inategemea na namana gani tunashughulika nayo.

2 Wakoritho 1:8-10 

Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi. Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu, aliyetuokoa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; ambaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa; 

Mateso na dhiki zilimfundisha Paulo asijitegemee Mwenyewe bali Mungu.Mungu ataendelea kuruhusu mateso ,dhiki, taabu,adha mbalimbali kwa watu wake pale wanapoanza kuwa wanajitegemea wenyewe na kushindwa kumtumainia Yeye.Ni kupitia mateso watu huwa wanaona kwa urahisi umuhimu na uhitaji wa Mungu.


Mwalimu Meinrald Mtitu




KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...