Tuesday, August 8, 2017

ZIJUE DHORUBA ZA MAISHA



Dhoruba Ni Njia Ya Mungu Kukujaribu Na Kuithibitisha Imani Yako


Mathayo 14:25-31

Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? 

Wakati Yesu anawajia akitembea katika maji,wanafunzi hawakuweza kumtambua.Walifikiri ni pepo au kivuli chake.Wakapiga kelele kwa hofu.Lakini Yesu alikuja na ujumbe wa amani na wa nguvu.Alikuwa na ujumbe wa Amani kwao.

Dhoruba za maisha zina uwezo wa kumfunua Mwokozi kwetu katika njia ambayo hatu kuzingatia kabla.Anapokuja kwetu,akitembea katika dhoruba zetu,hutupa ujumbe ule ule wa matumaini ambao waliwapa wanafunzi usiku ule.

Walikuwa bado wapo kwenye dhoruba pale alipo waambia wachangamke.Kwa uweza wake,Mwana wa Mungu anaweza kutupa amani katikati ya dhoruba zetu. Hii ni amani anayoitaja katika Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. 

Yesu alipojitokeza,alitokea akisema juu ya utambulisho wake, ”Ndimi”. “Mimi Ndiye”.Ni kauri kama ile aliyoisema kwamba Mimi Ndimi mlango,Mimi Ndimi njia ,kweli na Uzima,Mimi Ndimi mzabibu wa kweli,Mimi Ndimi mchugnaji mwema.

Yesu anawaambia wanafunzi wake wa furahi, Mungu yupo hapo.Tukiweza kuukamata ukweli kwamba Yesu ni Ndimi Mkuu na kwamba ana nguvu zote mbingu na dunia sawa na Mathayo 28:18,tunaweza kufarahia amani katikati ya majaribu.

Yesu analitoa ujumbe wa uwezo,alitioa amri kwa wanafunzi wake wasiogope.Tukiweza kuona ukweli kwamba Yesu anatawala kila eneo la maisha yetu,na kwamba ni Mungu ,na kwamba anazo nguvu zote,basi tunaweza kufika mahali ambapo tunaweza kumtumaini kabisa kupitia dhoruba zote za maisha.

Dhoruba za maisha ni Baraka kwasababu zinamfunua Mwokozi katika namna mpya kabisa.

Mathayo 14: 28-29,

Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. 

Dhoruba zinatutakasa.Pale Petro aliposikia kwamba ni Bwana alitaka kujiunga na Yesu kutembea katika maji.Yesu alimwambia tu Petro njoo.Petro aliitii na yeye akatembea katima maji.Yesu aliitumia dhoruba kama namana ya kumsaidia Petro kukua katika imani.

Pale dhoruba za maisha zinapotupiga kama tunataweza kuushika ukweli kwamba Yesu ni Bwana wa dhoruba,na sisi pia tunaweza inuka juu ya mazingira yetu na kutembea juu ya mawimbi na pamoja na Bwana.Dhoruba zinaweza kuinua viwango vyetu vya imani katika kumtumainia Bwana.

Natambua fika kwamba kutembea kwa Petro hakukudumu kwa muda mrefu.Punde alipoondoa macho yake kwa Bwana alianza kuzama.Hata hivyo,Petro ameacha ushuhuda ambao wanafunzi wengine hawakuwa nao.Ni yeye pekee anayeweza kusema niliwahi kutembea juu ya mawimbi.

Hakika Mungu anaweza kuzitumia siku zetu ngumu kutufundisha zaidi kumhusu Yeye na kutusaidai kukua katika Bwana.Atatumia mawimbi kukufanya uwe zaidi kama yeye.Kumbuka kulikuwa na watu kumi na mbili kwenywe mtumbwi lakini ni mmoja tu anayeweza kusema alitembea katika dhoruba kama Yesu.

Dhoruba Za Maisha Zinatukumbusha Ni Nani Ambaye Anatawala.

Mathayo 14: 30-31 

Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?

Petro alipotaka kutembea juu ya maji kama Yesu,Alimjaribu Bwana na akaingia katika maji.Hata hivyo pale alipotoa macho yake kwa Bwana na alipofanya hivyo alijikuta mwenywe kwenye matatizo. Lakini mara moja alikumbuka nani ambaye anatawala na akamwita Bwana na akapata masaada alio uhitaji.

Dhoruba za maisha zinatumika kutukumbusha sisi juu ya nani anayetawala.Kama Petro,kuna wakati tunaondoa macho yetu kwa Bwana wakati wa dhoruba zetu.Tunapofanya hivyo,tunajihakikishia kufeli au kushindwa.Tunahitaji kukumbuka nani ni msimamizi wa kila kitu.

Kama tutashinda na kufauli kwenye dhoruba za maisha hatustahili sifa kwamba ni kwa uwezo wetu au mafanikio yetu.Bali ni kwasababu kuna mmoja aliye mkuu kuliko sisi anaye tushika mkono. Mafanikio yetu na ushindi katika dhoruba za maisha yapo juu ya utayari wetu wa kutambua kwamba Yesu ni Bwana juu ya dhoruba.

KUZISHINDA DHORUBA KATIKA MAISHA YAKO


Pamoja na kuwa dhoruba katika maisha yetu sio nzuri, lakini bado zina tengeneza manufaa fulani katika maisha yetu.Kuna Baraka zilizojificha katika dhoruba za maisha zinazo tupiga sisi kama wana wa Mungu.Sijui ni aina gani ya dhoruba unayokabiliana ,lakini ninajua kwamba Bwana analo kusudi katika kuiruhusu dhoruba na tufani ipige katika maisha yako.


Mathayo 14:22,24

Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng'ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano. Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho.

Katika kifungu hiki cha maandiko,tunaona vile wanafunzi wa Bwana wakiwa wamekwama katika dhoruba kali.Walijikuta katika dhoruba ile,kwasababu walikuwa wameamriwa na Bwana kuvuka bahari ya Galilaya.Watu hawa walikuwa katika mapenzi ya Mungu na bado,wanaonekana wana hangaika katika dhoruba. Pamoja na kujitahidi kote,hata hivyo,inaonekana hawawezi kusonga mbele,Upepo unawapiga usoni .Watu hawa 12 wana kwamba katika dhoruba na washindwa kutoka. 

Je umewahi kujikuta katika hali kama hiyo? Umewahi kujikuta umekwama kwenye moja wapo mwa dhoruba za maisha,na haijalishi kiasi gani umejitahidi kujaribu, inaonekana umeshindwa kwenda mbele? Sawa,sote tuna nyakati kama hizo! Inaonekana kama dhoruba haitaisha na hakuna jema litakalo kuja kutoka kile tunacho kikabili.Hata hivyo pamoja na kuwa dhoruba katika maisha sio nzuri,zina tengeneza faida /manufaa fulani katika maisha yetu.

Dhoruba Ni Njia Ya Mungu Ya Kukujia na Kujifunua katika Maisha Yako. 


Mathayo 14:25-

Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.


Marko 6:48-

Akawaona wakitaabika kwa kuvuta makasia, kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho; hata ilipopata kama zamu ya nne ya usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; akataka kuwapita.


Yesu alikuja katikati ya majanga ya upepo makali na mawambi makali wakati wanafunzi walipokuwa wanapigania kuokoa maisha yao katika dhoruba.Napata picha kwamba hawa watu walikuwa wanaogopa juu ya maisha yao.Wakati walipofikiria kwamba matumaini yote yamekwisha na wamebaki bila matumaini,Upande wa pili Yesu anakuja akitembea katika mawimbi yale yale na upepo ule mkali akiwaendea.

Lile jambo ambalo wanafunzi waliogopa yaani bahari iliyochafuka,ndilo hilo hilo ambalo Mungu alilitumia kama njia cha kujifunua mwenyewe kwao.Atafanya hivyo hivyo katika maisha yako na yangu.Yesu aliwajia usiku bahari wakati wanaogopa.Biblia inasema Yesu aliwajia kwenye zamu ya Nne.Ambayo ni kati ya saa 9 na 12 Asubuhi,ni katika masaa ya giza ya usiku,Yesu alikuja kwao akitembea juu ya maji.

Jambo lile wanafunzi waliloliogopa,bahari iliyochafuka,ndicho kitu kile ambacho Mungu alitumia kuwaendea wao.Huu ni ushuda wa ajabu!Hakuwa anawaambia kwamba dhoruba haikuwa kali,alikuwa anawaambia kwamba alikuwa ni mkuu kuliko dhoruba.Hilo bado ni neno lake kwako! Pamoja na kile unachokikabili katika maisha,kumbuka Yesu ni mkuu kuliko dhoruba unayoweza kuwa unaipitia.

Unaweza kuwa unatembea katika giza na unashanga Yesu yupo wapi.Unaweza kuwa unazikabili siku fulani za giza katika maisha yako hata sasa.Ngoja nikukumbushe kwamba Mungu wetu yupo siku zote pamoja nawe sasa na Neno lake katika Waebrani 13:5 ambapo anasema, “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.” 

Ngoja nikukumbushe kwamba hata katika saa ya giza kabisa ya maisha yako Mungu bado ni Mungu na bado anatawala maisha yako. Hata saa ya giza sana ya maisha haiwezi kukuficha wewe kutoka katika uso wa Mungu.Yeye yupo hapo hata kama huwezi kumwona.


Mungu anaweza asikuzuie kuingika katika dhoruba,lakini atakutunza katikati ya dhoruba.

Kuna nyakati tunajihisi kama tumepoteza vita vyetu na dhoruba zetu,lakini wacha ni kukumbushe kwamba kama vile kwa hakika Bwana anatawala baraka zako.Yeye pia anatawala dhoruba zako.Wakati mambo yanaoneka ni mabaya kabasi,hebu angalia kukuzunguka,Yesu yupo karibu kujionyesha!Kumbuka anaweza asikuzuie kuingika katika dhoruba,lakini atakutunza katikati ya dhoruba.

Fikiria juu ya Vijana watatu wa kiebrania, Fikiri juu ya Danieli na Nuhu.Mungu hakuwazuia yeyote kati yahawa kuuingia katika dhoruba,lakini aliwaokoa wote kutoka katika dhoruba zao.Kile alichofanya kwao,atafanya kwako.

Kama utakuwa na subira na kumngojea, Yeye,atajionyesha katika wakati sahihi.Utaona vile Bwana atavyoitumia dhoruba kujiweka wazi kwako. Yaani kitu kile kile kinachokuogopesha kitakuwa ni chombo ambacho Bwana atakitumia kujionyesha na kujidhihirisha ukuu wake katika maisha yako.

Mungu alitumia dhoruba ya mwiba katika maisha yake Mtume Paulo ili kujionyesha na kujidhihirisha katika maisha ya Paulo.

2 Wakoritho.12:7-10.

Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu. 

Kile ninachojaribu kukuambia ni hiki: “ Usiogope dhoruba katika maisha! Dhoruba imesanifiwa na Bwana kama njia ya kumleta Yeye karibu kwako.Aliyazipanga na zipo kwaajili ya faida yako.”

Warumi 8:28 “ Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.”

Mungu Akubariki.

Tuesday, August 1, 2017

UKUAJI WA KIROHO






UKUAJI WA MAISHA YA KIROHO


Kukua kiroho ni maendeleo ya uhusiano wako na Mungu

Agano Jipya limeweka wazi kuwa mapenzi ya Mungu kila mwamini akomae kiroho. Mungu anataka sisi tukue.Neno ya kiyunani lenye maana ya “kukua” lina maanisha “ Kuongezeka,kuwa mwenye kuzaa zaidi au kuwa mkuu”. Wengine tunaposikia kukua kiroho tunaweza kujaribiwa na kufikiri hili jambo linawahusi wa Kristo wachanga walioamini hivi karibuni.Hivyo wao haliwahusu.

Kukua kiroho ni jambo linalomhusika kila mtu aliye mwamini Kristo.Bila kujali lini alifanya hivyo na haya ni mapenzi ya Mungu kwa kila mkristo.Mungu hataki sisi tubakie katika hali ile ile kiroho mwaka hata mwaka. Anatamani kutuona tunabadilika kutoka hatua moja ya utukufu kwenda nyingi mpaka tumegeuzwa katika sura ya Kristo.


Waefeso 4:14

“Ili tusiwe tena watotowachanga, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu...lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie Kristo”.


Mungu anataka kila mwamini awe na tabia ya Kristo.Swali kubwa kwa hiyo ni: Ni kwa namna gani kukua kiroho kunatokea? Tunawezaje kukua ndani ya Kristo?






Maana 7 Za Kukua Kiroho

1. Kukua kiroho ni mchakato wa kufanyika kuwa zaidi kama Yesu Kristo.


Lengo kuu la kukua kiroho ni kuwa kama Yesu. Mpango wa Mungu kwetu sisi tangu mwanzo ni sisi tufanane na Mwanawe. Kukua kiroho ni kubadilishwa kwako kuelekea kufanana na Yesu.

2 Wakorintho 3:18

Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho.

Warumi 8:29

Maana wale aliowajua tangu asili wafananishwe na mfano wa ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.

Tunapoweka imani zetu kwa Yesu,Roho Mtakatifu huanza machakato wa kutufanya kuwa kama Yeye,akitugeuza katika mfano wake.Kukua kiroho penginekunaelezwa vema zaidi katika 2 Peter 1:3-8, ambapo tunaelezwa kwamba kwa Nguvu za Mungu tunacho kila kitu tunachohitaji kuishi maisha ya utauwa ambalo ndio lengo la kukua kwetu kiroho.

Kila tunachohitaji kinatoka kupitia maarifa yetu ya Yeye,ambao ndio ufunguo wa kupata kila tunacho hitaji.Maarifa ya kumjua yanakuja kutoka kwenye Neno tulilopewa kwaajili ya kujengewa na kukua kwetu.


2. Kukua kiroho ni kuongezeka kwa tunda la Roho katika maisha yetu.


Kukua kiroho ni upanuzi wa kutegemea kwako katika kuenenda katika Roho.Kukua kiroho kunaainishwa na Tunda la Roho linavyo ongezeka na kuwa dhahiri katika maisha yetu.

Katika Wagalatia 5:19-23 kuona orodha mbili hapo.Mstari wa 19-21 kuna orodha ya “matendo ya mwili”.Haya ni mambo ambayo yalitambulisha maisha yetu kabla hatujaja kwa Kristo kwa Wokovu. Matendo ya mwili ni mambo ambayo tunaya ungamana na kuyatubu na kwa msaada wa Mungu tunayashinda.

Kadiri tunavyopata uzoefu wa kukua kiroho,ndivyo matendo ya mwili machache zaidi yatajionyesha katika maisha yetu.Kwa lugha nyingine ni kwamba kadiri tunavyi kua kiroho ndiyo matendo ya mwili yanavyi zidi kupotea katika maisha yetu.

Orodha ya pili ni ya Tunda la Roho hii ni mstari wa 22-23.Haya ni matendo ambayo yanapaswa kuwa ni tabia katika maisha yetu baada ya kuwa tunapata wokovu katika Kristo.Kadiri tunavyozidi kukua ndivyo nayo yanavyozikuwa dhahiri katika maisha yetu. 

3.Kukua kiroho ni kazi ya Mungu inayoendelea katika maisha ya muumini baada ya wokovu.

Kukua kiroho ni mwendelezo wa kilichofanyika katika wokovu, wakati maisha mapya yanapotolewa kwa muumini na kuwekwa ndani ya muumini.Kuna pande mbalimbali za ukuaji wetu. Roho Mtakatifu anatuhuisha ili kwamba tuweze kubadilishwa katika sura ya Mungu. Lakini mabadiliko haya ni hatua inayoendelea, na hatua hii inasonga mbele kwa ushirikiano wa Mungu na Mkristo.

Tumeambiwa katika


Wafilipi 2:12-13,

“utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka, kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yangu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.”



Hapa tunaona ushirika ambao ni lazima tufanye na Mungu. Hatuwezi kukaa tu bila kufanya kitu na kufikiri kwamba Mungu peke ataweka ndani yetu kumfanana kwetu. Lazima na sisi tujihusishe vilevile. Ni lazima “tufanye kazi.” Lakini kazi hii siyo ya kutufanya tukubalike na Mungu; isipokuwa ni kuonyesha kuelewa kwetu na kuonyesha shukurani ya msamaha wa dhambi zetu kupitia damu ya Yesu Kristo na kurithiwa kama watoto wa Mungu.


 4. Kukua kiroho ni hali ya mabadiliko ya wokovu kuchukua nafasi ndani yako.

Kukua kiroho ni hatua ya kuuvua utu wa kale na kuuvaa utu mpya.Wengine wanatazama kukua kiroho kama hatua ya kubadilisha utu wa kale wa dhambi kwa utu upya unaotokana na Kristo. Kadiri mtu wa kale anapokufa, mtu mpya anatokea. Wakati hii inapotokea, mtu anakua kiroho.

Pale mabadiliko ya wokovu yanapochukua nafasi ndani ya mwamini,kukkua kiroho huanza.Roho Mtakatifu hufanya makao ndani yetu.(Yohana 14:16-17). Sisi tu viumbe vipya ndani ya Kristo. Utu wetu wa kale wa dhambi unaanza kuacha njia kwaaji ya utu mpya ,Wenye asili ya Kristo.( 2 Kor.5:17, Warumi 6-7).Kukua kiroho ni mchakato mrefu wa maisha yote ambao unategeme na vile tunajifunza na kulitendea kazi Neno la Mungu na kutembea kwetu katika Roho.( 2 Timothy 3:16-17).


5. Kukua kiroho ni kukua katika ufahamu wa kumjua Mungu
Kumjua Mungu ndiyo kusudi na maana ya uzima wa milele. Kisa hasa cha kutaka maisha ya kikristo inatakiwa iwe kumjua Mungu katika kweli. Kwa hiyo, tunapoendelea kukua kumjua yeye katika ukuu wake wote, tunakua kuwa kama yeye.
Nafasi ya kwanza ya utaratibu wa ukuaji inahusisha kukua katika mwanga wa Mungu. Katika Yohana 17:3 Yesu anasema, “Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo aliyetumwa.”

Kadiri tunavyokua katika kumjua Mungu, ndivyo tunavyobadilishwa zaidi na zaidi kuwa katika mfano wake.Ufunguo wa kumjua Mungu ni kuelewa tabia yake ya utakatifu. Tunajifunza kuhisi kama mtume Paulo alivyosema, “Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu” (Wafilipi 3:8a). Hii ni sehemu ya hatua ya utakaso.

Tunapokuwa tunakua katika mwanga wa Mungu katika ukamilifu wake wote, tunakua na kujitambua wenyewe pia. Kipekee, tunafikia kujua hali yetu ya dhambi tofauti na tabia kamilifu ya Mungu. Kadiri tunavyomsogelea karibu Mungu, ndivyo tunavyojiona kuwa mbali naye. Kadiri tunavyomjua alivyo mtukufu kweli, ndivyo kadiri dhambi zetu zinavyodhihirika mbaya zaidi kwetu.


Yeremia 9:23-24

“Bwana asema hivi, mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake, bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifamu mimi na kunijua ya kwamba mimi ni Bwana, nitendaye wema na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo , asema Bwana”


6. Kukua kiroho ni mchakato wa kufanyika kuwa Mwanafunzi wa Yesu.

Biblia inatufundisha kwamba Waamini waliokomaa ndio wanaoitwa wanafunzi.Hili ni Neno ambalo Biblia linatumia kwa waamini waliokomaa tu.Mtu hawezi kuwa mwanafunzi bila ya kuwa chini ya nidhamu.Maneno mwanafunzi na nidhamu yana kwenda pamoja .Disciple – discipline.kadiri ninavyo kuwa nimetiwa nidhamu ndivyo nitavyotumiwa zaidi na Mungu.

Alama ya uanafunzi ni kubeba Msalaba.Mungu anatutaka sisi kubeba Misalaba yetu.Luke 14:27, Luke 9:23.Msalaba huo unabebwa kila siku na kumfuata kila siku.Kubeba msalaba kuna husisha kufanya chochote kila ambacho kitamfanya Kristo kuwa na nafasi ya kwanza katika maisha yangu.


7. Kukua kiroho ni kukua katika Utakatifu wake.


Baada ya kumjua Kristo kama mwokozi, tunatakiwa tuendelee kukua katika mwanga wetu wa utakatifu wa Mungu na katika utambuzi wa hali zetu za dhambi. Hii inaweza kuwa uzoefu wa kuhofisha.
Kumjua Mungu na Utakatifu wake ni kukaribisha kujiweka wazi wenyewe, na huu ni uzoefu wa kutisha kwa hao wanaopenda kuficha makosa yao na mapungufu. Kwa jinsi hiyo, kwa mkristo anayekua, pengo linaonyesha hitaji la kuendelea kumhitaji Kristo na ukuu wa yale aliyofanya msalabani

Kadiri tunavyomjua Mungu ndivyo kadiri tunavyojiona kutofaa mbele zake. Mwanga huu unapokua,tunaona maana ya msamaha wetu na upatanisho wetu kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.

Tunapoufahamu ukuu wa Mungu, (kama Isaya alivyofanya alipoona utukufu wa Mungu hekaluni, au kama taifa la Israeli walivyofanya walipokutana na Mungu katika mlima Sinai). Tunagundua utukufu wa kweli wa mwokozi. Damu yake inaosha wenye dhambi na kuzisafisha na kutuvalisha mavazi meupe ili kwamba tuweze kumsogelea Mungu huyu wa utukufu.


Pastor Meinrald Mtitu.

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...