Friday, September 15, 2017

TABIA KUMI ZA MTU MVIVU




TABIA KUMI (10)  ZA MTU MVIVU

1. HUPENDA SANA USINGIZI NA KULALA KWA MUDA MREFU.

MITHALI 19:15- Uvivu huleta usingizi mzito, naye mtu mzembe huona njaa.

Kulala ni jambo la kawaida na la muhimu kwa kila mwanadamu. Kwaajili ya afya njema ya mwili na akili tunahitaji wastani wa masaa 6-8 ya kulala.Hakuna tatizo katika kulala ,tatizo ni pale kulala kunapo tumika kama kichaka cha kujifichia na kukwepa kufanya kazi.

MITHALI 26:14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.

Mtu mvivu huona vigumu sana kukiacha kitanda chake. Anapenda sana kulala kupita mahitaji ya kawaida ya mwili wake. Watu wenye uvivu uliojificha ndani yao wakiugua kidogo au kujisikia vibaya kidogo basi kitanda kita wakoma siku hiyo ,hawatatoka kitandani.

MTIHALI 6:9-10 Ewe mvivu, utalala hata lini? utaamka lini kutoka katika usingizi wako? Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono upate usingizi!

Kuna uvivu uliojificha nyuma ya kupenda kulala sana kupita mahitaji ya kawaida ya mwili na akili.

MITHALI 20 :13

Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.


Wako watu wavivu wanaokesha usiku wanaangalia luninga kiasi kwamba asubuhi hawezi kuamka,mchana kutwa wanashinda wamelala. Hii ni tabia ya uvivu. Wako watu wavivu ambao wanapenda mno usingizi kiasi kwamba hata wakijitahidi kutega kengele ya saa (Alarm) iwaamshe bado hawawezi kuamka. Wako watu wanaochelewa mara kwa mara kazini, shuleni au kuwahi usafiri kwaajili ya safari n.k.sababu kubwa ni uvivu uliojificha katika kupenda usingizi.


2. HUWA MLEGEVU KATIKA KAZI NA KUUPOTEZA MUDA KWA MAMBO YASIYO NA TIJA.


MITHALI 18:9

Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu...


Tabia nyingine ya mtu mvivu ni kupoteza muda,hajali muda kabisa. Katika zama hizi za teknolojia moja ya vitu vinavyo poteza muda ni pamoja matumizi ya mitandao ya kijamii kupitia simu za kisasa za “ Smart phone”, Michezo ya kwenye simu na komputya, vipindi vya televisheni hasa vile vya maigizo na filamu.Eneo jingine ni lile la kuwasiliana kwa simu maarufu kama ku-chat.

Kwa kuwa watu wengi walio wavivu hawana nidhamu binafsi ni rahisi sana kutekwa na kutumia muda wao mwingi sana katika maeneo hayo tena hata wakiwa kazini.

Kutumia masaa mengi kawa mambo yasiyo na tija sio tatizo kwa mtu aliye na uvivu uliojificha,haoni ni tatizo lolote kuwa katika makundi ya mitandao ya kijamii na kutumia muda wake wote huko.Hata kama ni makundi ya kujadili Biblia na mambo mengine ya manufaa, haingii akili kuona mtu yupo online na akijadiliana na kubisha kuhusu Biblia kwa masaa sita! Hivi huna mambo mengine ya kufanya?

MITHALI 14:23 Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida, bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.
Mtu mvivu utamwona yupo kwenye makundi karibia kumi ya facebook na whatsApp ,bado yupo kwenye mitandao ya Instragram,Telegram, Jamii Forum na mingineyo, na kila kundi kuna mada fulani inaendelea na anataka ashiriki kuchangia.Atafanya kazi saa ngapi?atafikiri saa ngapi?

Wavivu wengine wapo ofisini utaona wakati wote wapo kwenye mitandao,unafanya kazi saa ngapi? Huo ni ulegevu na uvivu! Kuna vitu vya muhimu zaidi katika maisha zaidi ya kuwa muda wote kwenye facebook ,Instragram na Twitter.

Kuna watu ukiwaachia kazi ya kufanya hawezi kuifanya kazi na kuikamilisha kwa wakati kwasababu muda wao wote wanaupoteza kuzungumza,kupiga stori,na mazungumzo yenyewe ni yale ya upuuzi tu.Wengine ni kupoteza muda wote kwenye simu,watapigia watu simu hata kama hawa jambo lolote la maana kwasababu tu amejiunga na kifurushi cha bei nafuu na ana muda hewani wa kutosha.Huu nao ni uvivu.



3. HUACHA MAMBO YANA HARIBIKA BILA KUCHUKUA HATUA.

MITHALI 24:30-31

Nilipita karibu na shamba la mtu mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili, miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.




Mtu mvivu hawawezi kutengeneza vitu vinavyo haribika .Watu wavivu wanatabia ya kuacha mambo yanaharibika bila ya kuchukua hatua hata kama jambo husika lipo katika uwezo wao kulirekebisha.Wana acha hata nyumba zao zina haribika na kuvuja bila kufanya marekebisho kwa wakati.Mambo madogo ambayo wangeweza kuyashughulikia yataachwa hivyo kwa muda mrefu.

Nguo inaweza kubaki imechanika au kutatuka mahali bila ya kushonwa kwa muda mrefu tu kitu ambacho ni kidogo sana.Wengine kurudishia kishikizo tu kwenye shati inaweza kuchukua miezi na anaendelea kulivaa!Wengine ni viatu vilivyotatuka vitaendelea kuvaliwa bila marekebisho.

MHUBIRI 10:18

Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.


Kushindwa kufanya marekebisho na matengenezo madogo madogo tu ni dalili ya uvivu uliojificha. Hii inaendana na tabia nyingine ya kuahirisha mambo tutayoiangalia hapo mbele.



4. HUJAA UDHURU WA KUAHIRISHA MAMBO BILA SABABU ZA MUHIMU.

MITHALI 22:13

Mvivu husema, ‘‘Kuna simba nje!’’ au, ‘‘Nitauawa huko njiani.


Watu wavivu hutafuta sababu za kipuuzi za kutoka kufanya kazi. Wamejaa udhuru na “visababu” vya kuwepa kufanya kazi.Nyuma ya sababu zao kuna uvivu “ uliojificha”.Wakati wote wanatafuta udhuru wa kipuuzi wa kutofanya kazi na hawaukosi!


MITHALI 26:13

Mvivu husema, ‘‘Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”



Ukimpa kazi mtu mvivu hatakosa sababu ya kutoikamilisha. Kwa kila sababu unayompa ya kufanya kazi,yeye atakupa sababu mbili ya kwanini asifanye kazi hiyo. Mtu mvivu si wakuachiwa kufanya jambo,mwachie mtu mvivu na hakuna kitu kitafanyika.

Kauri mbiu ya watu wavivu ni “kamwe usifanye leo lile unaloweza kuliacha mpaka kesho”. Watu wavivu ni wepesi kughahiri jambo na kuahirisha jambo tena bila sababu.

Mtu mvivu huwa haheshimu na kufuata ratiba aliojiwekea mwenyewe. Kuna ushauri wa hekima unasema “Usiache lifanyike kesho lile unaloweza kulifanya leo”.Ingawa ,watu wavivu wao wanasema“Kwanini ufanye leo lile unalo weza kufanya kesho?”


MITHALI 20:4

Mvivu halimi kwa majira, kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati cho chote.


Mtu mvivu anaweza kujitetea kuna joto sana au kuna baridi sana , ingawa wengine wote wanafanya kazi katika hali hiyo hiyo ya hewa.Anaweza akaacha kufanya kazi kwa hofu ya kuumia,ingawa uwezekano wa kuumia ni mdogo sana au haupo kabisa.

MITHALI 26:16

Mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wajibuo kwa busara.


Katika Mathayo 25.kuna mfano wa Talanta,Bwana aliyesafiri kwenda nchi ya mbali aliwapa watumishi wake talanta (fedha za wakati huo) ili wazizalishe mpaka atakapo rudi.Wawili walifanya fanya bidii na kuzalisha,lakini mmoja hakufanya kitu alifukia talanta aliyopewa.Na Bwana wake aliporudi alitoa sababu za kipuuzi kwanini hakuzalisha fedha aliyoachiwa hebu sikia sababu zake za kipuuzi .

MATHAYO 25:24-29:

“Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba wewe ni mtu mgumu, unayevuna mahali usipopanda na kukusanya mahali usipotawanya mbegu. Kwa hiyo niliogopa, nikaenda, nikaificha talanta yako ardhini. Tazama, hii hapa ile iliyo mali yako.’

“Bwana wake akajibu, ‘Wewe mtumishi mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna mahali nisipopanda na kukusanya mahali nisipotawanya mbegu. Vema basi, ingekupasa kuweka fedha yangu kwa watoa riba, nirudipo, nichukue ile iliyo yangu na faida yake?


‘‘ ‘Basi mnyang'anyeni hiyo talanta mkampe yule mwenye talanta kumi.’Kwa maana kila mtu mwenye kitu ataongezewa, naye atakuwa navyo tele. Lakini kwa mtu yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa.

Sababu anazozitoa ni za kipuuzi,nyuma ya sababu hizi zote ni uvivu tu ndio ulikuwa tatizo lake.Huyu mtumishi mvivu hakujua kuwa ukiweka fedha aridhini haiwezi kuota. Alipaswa kujaribu hata kuweka benki,angepata riba kuliko kuto fanya chochote.Na Yule Bwana alimwita ni mwovu na mvivu.


5. HUSUBIRI MPAKA MAZINGIRA YAWE SAHIHI NDIPO AFANYA KITU.



MITHALI 19:24

Mtu mvivu huuzamisha mkono wake kwenye sahani, lakini hawezi hata kuurudisha kwenye kinywa chake!


Watu wavivu hawana msukumo na motisha ya kufanya mambo. Watasubiri mpaka mazingira yote yawe sahihi ,yawe vizuri ndipo utawaona wanashughulika .Baadhi ya watu wavivu hawana hamasa kabisa na kazi,hawana tamaa ya kufanya mambo makuu ndani yao.

Kuna watu waliozaliwa au kukulia katika mazingira ambayo ni rahisi kuwafanya kuwa wavivu.Wananunuliwa kila kitu,hawajajifunza kuzalisha chochote kwa nguvu zao,hawawezi kuchuma wao wenyewe. Wamezoea na kujifunza kusubiri mtu mmoja awape mkononi !

MITHALI 26:15 Mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye hushindwa kuurudisha tena kinywani mwake.


Ni vizuri watoto wafundishwe kazi wakiwa bado wadogo wasifanyiwe kila kitu! Wapo watoto wamekuwa hawajui hatakufua soksi zao tu! Kila kitu walikuwa wanafanyiwa.



6. HUTUMIA VIBAYA KILE ALICHONACHO.


MITHALI 12:27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.

Mtu huvivu atapanya na kufuja kile alichonacho.Mtu mvivu hawezi hata kukitunza kile alichonacho.Uvivu wake utamfanya hata kile alicho nacho kiharibike kabisa na kuchakaa .

MITHALI 24:30-31

Nilipita karibu na shamba la mtu mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili, miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.


Kuna baadhi ya vitu haviwafahi kabisa watu wavivu, hasa vile vinavyohitaji usimamizi na uangalizi wa karibu na marekebisho ya mara kwa mara. Ukiwapa hesabu ni hasara tupu. Kuna watu wanakaa na chakula mpaka kinaharibika kwaajili ya uvivu wa kukipika tu.

Kuna watu wanaacha nguo kwenye maji mpaka zinaharibika kwaajili ya uvivu wa kuzifua tu.Kuna watu wanaacha shamba lina haribika kwasababu ya uvivu wa kulipalilia kwa wakati.

MITHALI 18:9 Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu.

Watu wavivu ni waharibifu wa vitu,wape kazi yako wataiharibu tu.

7. HUTAMANI MAMBO MENGI LAKINI HAWEZI KUZALISHA.

MITHALI 21:25-26 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi. Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.

Watu wavivu wanazao shauku na matamanio lakini hawezi kuzitimiza. Hata wakiwa na ndoto haziwezi kutimia.Wavivu wengi wanaota ndoto za mchana wakiwaza kuwa na mambo makubwa lakini hayatakamilika maishani mwao.

MITHALI 26:15 Mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye hushindwa kuurudisha tena kinywani mwake.

MITHALI 19:24

Mtu mvivu huuzamisha mkono wake kwenye sahani, lakini hawezi hata kuurudisha kwenyekinywa chake!

8. HAKUBALI KUTAMBUA KWAMBA YEYE NI MVIVU

MITHALI 26:16

Mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wajibuo kwa busara.

Watu wavivu huwa wakubali kwamba wao ni wavivu,wana hekima machoni pa wenyewe.Hata mtu mvivu hapendi na anachukia akiambiwa wewe ni mvivu. Watu wavivu si waanzishaji wa mambo ,watasubiri wengine waanzishe na wao hatimaye wahamasike.Watu wavivu hatawakianza jambo huwa hawalimalizi,wana weka mambo mengi viporo.Wanaweza kuwa na mipango mingi lakini yote haikamiliki.

Watu wavivu si waanzilishaji wa mambo na hawamalizi yale wanayoanza. Wana maisha yalivugurukika yasiyo na mpangilio.Maisha ya watu wavivu hayana mpangilio,wana maisha yaliyo vurugika.



9. HUPENDA KUWA TEGEMEZI NA KULEMEA WATU WENGINE.


2 WATHESALONIKE 3:8

wala hatukula chakula cha mtu ye yote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu ye yote miongoni mwenu.


Watu wavivu wanapenda vitu vya bure ,wanakwepa kugharimika. Wengi wanatabia za kuwalemea watu wengine na kugeuka mzigo.Watu watakusaidia lakini uje pia watu watakuchoka.Wako watu wana tabia ya kuomba omba vocha za simu,nauli na vitu kama hivyo mpaka watu wanawachoka.Kuna msemo unasema; “hakuna chakula cha bure,kile unachokiona ni cha bure ujue kuna mtu mwingine amekilipia gharama.”

I Wathesalonike 4:11-12

Jitahidini kuishi maisha ya utulivu, kila mtu akijishughulisha na mambo yake mwenyewe na kufanya kazi kwa mikono yake, kama vile tulivyowaagiza, ili maisha yenu ya kila siku yajipatie heshima kutoka kwa watu walio nje, ili msimtegemee mtu ye yote.


10. HUFANYA KAZI ZAKE KWA ULEGEVU NA UZITO.
MITHALI 18:9

Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu...


Mtu mvuvi hufanya kazi kwa uzito,kazi ya kuchukua muda mfupi na siku chache kwa mtu mvivu itachukua muda mrefu na siku nyingi bila sababu za msingi.Mtu mvivu ni goigoi,anajivuta sana katika kufanya shughuli zake.



Mwalimu M.A.MTITU




1 comment:


  1. WELCOME TO THE GREAT BROTHERHOOD.
    Do you want to be a member of Illuminati as a brotherhood
    that will make you rich and famous in the world and have
    power to control people in the high place in the worldwide
    .Are you a business man or woman,artist, political,
    musician, student, do you want to be rich, famous, powerful
    in life, join the Illuminati brotherhood cult today and get
    instant rich sum of. 2 million dollars in a week, and a free
    home.any where you choose to live in this world
    BENEFITS GIVEN TO NEW MEMBERS of ILLUMINATI.
    1. A Cash Reward of USD $500,000 USD
    2. A New Sleek Dream CAR valued at USD $300,000 USD
    3.A Dream House bought in the country of your own choice
    4. One Month holiday (fully paid) to your dream tourist
    destination.
    5.One year Golf Membership package
    6.A V.I.P treatment in all Airports in the World 7.A total
    Lifestyle change 8.Access to Bohemian Grove
    account every month as a member
    9.One Month booked Appointment with Top 5 world
    Leaders and Top 5 Celebrities in the World.
    If you are interested of joining us in the great brotherhood of illuminati CONTACT MR ROLAND or WhatsApp him +2348142587627
    or email:illuminatipower666brotherhood@gmail.com

    ReplyDelete

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...