Wednesday, June 28, 2017

KUWA MSHINDI KAMA MTENDE

KUWA  MSHINDI KAMA MTENDE

“Matawi ya mti wa  mitende hutumika kama ni Alama ya ushindi      na furaha”

ZABURI 92:12-13
Mwenye haki atasitawi kama mtende, Waliopandwa katika nyumba ya Bwana Watasitawi katika nyua za Mungu wetu.

    M
tende ni mti unaobeba alama ya mafanikio na ushindi. Kwa miaka mingi matawi yake yametumika kuonyesha alama ya ushindi furaha na Amani.Mara nyingi katika Neno la Mungu kila mahali matawi ya mitende yalipo tumika yalihusianishwa na ushindi.
 Mfano Kwenye hekalu la Sulemani Tunaona mitende ilikuwa ni moja ya michoro iliyokuwepo kwenye hekalu la Sulemani ikiashiria ushindi.Matawi ya Mitende tunaona yakitumika kumshangilia na kumwimbia Yesu alipokuwa anaingia Yerusalemu.

YOHANA 12:12-13

Siku iliyofuata umati mkubwa uolikuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu. Basi wakachukua matawi ya mitende wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana! Amebarikiwa Yeye ajaye kwa Jina la Bwana! Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!’’

Katika Kitabu cha UFUNUO 7:9-10 tunaiyona mitende ikitajwa na ikieleza vile Watakatifu  walio vaa mavazi meupe wakiimba kwa ushindi mkuu wakiwa wameshika matawi ya mitendi mikononi mwao  wakiashiria Ushindi.

“Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao;”

KWELI YA KIROHO:
Mungu anawafananisha wenye haki na miti ya mitende kwasababu anawataka wawe na maisha ya Ushindi.Wenye haki ni washindi ndani ya Kristo.Ndani ya Kristo Wanashinda na zaidi ya kushinda.

Biblia inatumia majina mengi kuwaelezea wale walio ingia katika maisha  ya uhusiano binafsi na Bwana Yesu Kristo,moja ya majina hayo wanaitwa ni Washindi.Hiki ni cheo ambacho Yohana anakitumia katika nyaraka zake.

 I Yohana 5:4
Kwa maana kila aliyezaliwa na Mungu huushinda ulimwengu. Huku ndiko kuushinda kuushindako ulimwengu, yaani, hiyo imani yetu”

Mtume Paulo naye anawaeleza wale walio mwamini Kristo kama ni watu walio washindi na wenye ushindi katika mambo yote.

WARUMI 8:37
Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda

Mshindi Ni Nani ?

Mshindi kwa kiingereza overcomer katika maana ya kawaida  ya lugha ya kiyunani “nikao” ni victor, pia tunapata neno nike. Ambalo  wayunani walilitumia kama jina la mungu mke wa Ushindi. Katika Imani zao waliamini ushindi unapatikana kwa miungu tu na sio wanadamu,miungu tu ndio ilikuwa washindi na walikuwa hawashindwi.

Kwa maana kila aliyezaliwa na Mungu huushinda ulimwengu. Huku ndiko kuushinda kuushindako                           ulimwengu, yaani, hiyo imani yetu.-       
Mtume Yohana,” 100 A.

Sisi tu washindi wa wokovu,ni wale tu waliozaliwa na Mungu ndio washindi wa kweli.Ushindi wetu ni kwasababu tu tupo ndani ya Kristo aliye mshindi.Yesu alitumia neno hili nikao katika Yohana 16:33 pale aliposema kwa maana Mimi nimeushinda ulimwengu.’’ Ni neno Mshindi.Yesu alikuwa anasema kwamba ameushinda mfumo wa Shetani.


Ukweli kuhusu maisha ya Mkristo ni kwamba yupo ndani ya Kristo,hawezi kutenganishwa katika Muungano wake na Kristo mwenyewe hivyo yu mshiriki wa asili ya uungu.Mkristo anashiriki kila kitu alicho nacho Kristo, Hii ni pamoja na urithi,haki,mauti,uzima na Roho.Kwa vile Kristo ni mshindi  na Mwamini pia ni Mshindi.Wale walio zaliwa na Mungu ndio washindi wa kweli.

Tuesday, June 27, 2017

KUPANDWA KAMA MTENDE


KUPANDWA KAMA MTENDE

“Wenye haki wanafananishwa na mitende iliyopandwa  katika  uwanja wa nyumba ya Bwana”

Zaburi 92:13
Waliopandwa katika nyumba ya Bwana Watasitawi katika nyua za Mungu wetu.


    M
ti huu katika Zaburi hii sio wakaida kwasabu ya mahali ulipo.Umepandaka uwanja katika Nyumba ya Bwana.Hekalu katika Yerusalemu  lilikuwa ni Nyumba ya Mungu ambapo aliishi kati ya watu wake.Na kulikuwa na eneo la uwanja ambako mti ulipandwa pale.

KWELI YA KIROHO:

Kama wewe ni mwenye haki Zaburi inatuambia kwamba  wewe ni kama  mfano wa mti Wenye  nguvu na afya uliopandwa katika nyua au uwanja wa nyumba  ya Mungu.

Kweli Tano  (5 )kuhusu  kupandwa nyumbani  Mwa Bwana:
1.      Kupandwa Nyumbani mwa Bwana kunatufanya tuwe wenye haki.

Neno kupandwa lililotumika hapo, kiebrania ni Shathal  ambalo kwa  lugha ya kiingereza ni “to be transplanted “,yaani kuhamishwa na kupandwa mahali pengine. Hivyo ni kusema wenye haki wamehamishwa kutoka mahali pengine na kuja kupandwa kwenye uwanja uliopo katika nyumba ya Bwana.

Katika hali ya kawaida mti hauwezi kupandwa katika nyumba ya Bwana,kama umepanda katika uwanja nje ya jengo basi kuna mtu ameuhamishia hapo toka ulipo kuwa na kuupanda .
Hii ni picha ya kutuonyesha vile ambavyo kuwa mwenye haki si kitu kinafanyika kwa nguvu zako mwenyewe,si wewe unayejifanya kuwa mwenye haki,sio juhudi zako,ni Mtu mwingine anaye kuhamisha na kupanda upya na kukufanya mwenye haki.

Katika hali ya kawaida mti haumei au kuota ,katika nyumba Bwana.Hata sisi hatukuanzia nyumbani mwa BWANA ,tulihamishwa kutoka mahali kwingine na kupandwa, kwa kwaida  na kwa asili si wanyumbani mwa Bwana. Huwezi kuwa mwenye haki  mpaka uhamishwe na kupandwa huko.
2.      Kupandwa nyumbani mwa Bwana kunatufanya kuwa hai kiroho
Mti wa mtende unaotaja kwenye zaburi ni mti ulio hai,unaishi. Wenye haki kwa mfano wa mtende wako hai kiroho Ni wenye haki peeke yao walio hai kiroho.Wasio haki hawako hai kiroho,ni wafu.
Kama ambavyo huwezi kupandikiza mti usio na uhai,unapandikiza mti wenye uhai ,kwa namana hiyo hiyo mwenye haki ana uhai ndani yake,Sio tu ni hai kimwili bali ni hai kiroho.Mungu ndiye chanzo cha uzima wake.( Waefeso 2:5)
3.      Kupanda nyumbani mwa Bwana kunatufanya tuwe  na mahusiano ya karibu na Mungu
Kila mtu uliokua katika uwanja wa hekalu lazima uwe umeleta kutoka mahali pengine na kupandikizwa.Na hauwezi kujipandikiza wenyewe n lazima mtu mwingie aupandikize. Kwa jinsi hiyo hiyo Mungu anatufanya wenye haki.Mungu si tu ametupa uzima na kutufanya hai kiroho lakini pia ametuleta karibu naye katika mahusiano.
Mungu ametutoa mbali na kutuleta kutupanda katika nyumba yake,mahali ambapo yeye yupo.Hii ni picha ya mahusiano ya karibu ya Mungu baada ya kufanywa kuwa wenye haki wake ,Mungu amtuleta karibu naye kiroho.(Waefeso 2:13, Wakolosai 1:13)

4.      Kupandwa nyumbani mwa Bwana kunatufanya tuwe katika mahali pa heshima na utukufu.
Kuna maeneo ya heshima ambako mti ukipandwa hapo ni sehemu maalumu sana.Si kila mahali pana weza kuupa mti hadhi.Kupandwa kwa mti wa mtende nyumbani mwa Bwana ,katika eneo la hekalu ni heshima kubwa.Hekaluni ni mahali pa heshima na utukufu.Si mahali kama mahali pengine pa kawaida.Hekaluni palikuwa ni Nyumba ya Mungu duniani,palikuwa ni mahali uwepo wa Mungu hapa duniani katikati ya watu wake wa agano.
Kitendo cha kuwa mwenye haki ni kitendo cha kupewa heshima kubwa,ni kama mtende uliopanda hekaluni mahali pa heshima kubwa.Kuwa mwenye haki ni kupatanishwa na Mungu kupitia Yesu Kristo.Ni kuingizwa na kuasiliwa katika familia ya Mungu.Tuna mahali pa heshima kama mtende uliopandwa kwenye nyua za Bwana.
5.      Kupandwa nyumbani mwa Bwana ni kuwa katika mahali pa Ulinzi na usalama.
Mti uliopandikizwa katika nyua ,viwanja vya hekalu una usalama na ulinzi mkubwa.Mti huu utalindwa dhidi ya kuwa wazi na kupigwa na upepo makali.Mti huu utalindwa na kukatwa na watu kwaajili ya kuutumia kama mbao au kuni.Nyuani mwa Hekalu ndipo mahali salama kabisa Ulimwenguni kwa mti kuwa.
Hii ni picha ya kupendeza ya usalama na ulinzi wa Mwenye haki wa Mungu.Ukweli huu ni kwetu pia,kila ambaye ni wa Mungu ndani ya Kristo yupo salama. Unapokuwa ni wa Mungu,macho yake yanakutaza siku zote.Upendo wake unakuzunguka.Na unakuwa salama dhidi ya wale wanaotaka kukudhuru,Hawawezi kukudhuru.
Katika Yohana 10 Yesu anazungumza juu ya usalama tuliona nao kwake.Paulo anzungumza hakuna kitu cha kututenganisha na upendo wa Kristo.

Mchungaji na Mwalimu,M.A.Mtitu
Ligh of Hope Teaching Ministries

Sunday, June 25, 2017

MWENYE HAKI KAMA MTENDE

M
aisha yetu ya kiroho ni jambo la kuwekewa uzito mkubwa kuliko jambo jingine lolote.Tunapaswa kuyajali maisha yetu ya kiroho zaidi ya mambo mengine maana hapo ndipo uhusiano wetu na Mungu ulipo na ndipo maana na makusudi ya maisha ilipo.

Mungu  katika Neno lake katika Zaburi 92:12-14 anayafananisha maisha ya Mwenye haki na mti wa mtende. Kama vile mtende unavyostawi na kuchanua wakati wote na kuzaa matunda ndiyo  maisha yetu ya kiroho yanavyotarajiwa yawe  na ustawi na mafanikio, afya na ubora.

Kuna hazina kubwa na  utajiri na  katika  kila mstari ulio katika Biblia ikiwa utachukua muda kutafakari na kumruhusu Roho Mtakatifu akuangazie.

Unaweza kujiuliza maswali kama mimi nilivyojiuliza wakati naitafakari mistari hiyo.Kwanini Mungu anamfananisha mwenye haki na Mti wa mtende? Kuna nini cha tofauti au cha kipekee sana katika  mti wa  Mtende ambacho kinalingana na kufananishwa na mtu mwenye haki? Ni kwa njinsi gani mti wa mtende una kua na  unastawi? Na maswali mengi kama hayo.

Ili kupata majibu ya maswali hayo na mengine mengi  ilinilazimu kuanza kufanya tafakari ya kina ambayo nilifanya kwa  kipindi kirefu juu ya mistari hiyo



ZABURI 92:12a
                                                                                                                                                                                                                          “Mwenye haki atasitawi kama mtende”

“Mungu ametumia picha ya  mti wa Mtende  kumfananisha  na mtu mwenye haki”

    N
eno  “mwenye haki” sio neno linalosikika vizuri masikioni mwa baadhi ya  watu.Kama mtu atakuita  “mwenye haki” unaweza usijisikie vizuri  na kushituka.Pengine usingejali sana  kama ungeitwa “mtu mwema”, “Mtu mzuri” na majina mengine kama hayo lakini sio kutiwa  “mwenye haki”. Kwa namana fulani jina hili linashitua.

Sababu kubwa ni kwamba neno  “mwenye  haki” linatukumbusha juu ya “kujihesabia haki.” Mtu mwenye kujihesabia haki ni yule ambaye anafikiri  anaweza kujifanya mwenyewe kuwa mwenyewe haki kwa matendo yake fulani mazuri na mema anayotenda.Mara nyingi anajifikiria na kujiona yeye ni bora kuliko wengine wote. Ni kama vile mafarisayo walivyokuwa.

KWELI YA KIROHO;
Kama ambavyo mtende uliopandwa nyumbani Bwana na kustawi  ndivyo yalivyo maisha ya mtu ambaye ana Ana mahusiano na Mungu na amehesabiwa haki na kufanywa mwenye haki wake.

Maana ya  kuwa Mtu Mwenye haki

Biblia inapotumia neno mwenye haki haina maana hiyo.Hivyo hatupaswi kulikwepa neno hili au kujisikia vibaya linapoitwa kwetu, Mungu mwenye amelitumia  kwa watu wake.Katika Agano la kale neno hili limetumika sana kuwaelezea watu wanao mcha Mungu.

Mtu yule ambaye amedhamiria moyoni mwake kumcha Mungu wa kweli, huyo ndiye anaitwa mwenye haki.

Kuwa  mtu mwenye haki katika muktadha wa kibiblia  ni kuwa kinyume cha mtu mwovu.Na unaweza kuwa mwenye haki bila ya kujihesabia haki.Kuwa mwenye haki ni sawa na kuwa mtu mtauwa.Ni kitu ambacho sisi   sote tunapaswa kutamana kuwa. Mtu yule ambaye amedhamiria moyoni mwake kumcha Mungu wa kweli, huyo ndiye anaitwa mwenye haki.

Mungu ndiye mwenye kutuhesabia haki na kutuita wenye haki.Watu waliomcha Mungu wakati wote walijua kuwa hawajawa wenye haki kwa  juhudi zao wenyewe.Walijua kuwa haki yao inategemea kabisa Neema ya Mungu.

Mungu anatupa picha ya mwenye haki na ahadi alizonazo mtu mwenye haki  ambaye amemfananisha na mti wa mtende na mwerezi.Katika somo hili tuna angalia zaidi picha ya mwenye haki kama mti wa mtende.

Kitabu cha Mithali na Zaburi ni vitabu ambavyo vinaonyesha faida za kuwa mwenye haki ,na mara nyingi vimefanya ulinganifu baina ya mwenye haki na asiye haki au mwovu.

Katika Zaburi 92 kabla ya Mungu kutupa picha ya Mtu mwenye haki  yupo vipi ana anza kwanza  na kutupa picha ya mtu asiye haki vile alivyo.
Zaburi 92:7
Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele;


MUNGU AKUBARIKI.

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...