Tuesday, August 1, 2017

UKUAJI WA KIROHO






UKUAJI WA MAISHA YA KIROHO


Kukua kiroho ni maendeleo ya uhusiano wako na Mungu

Agano Jipya limeweka wazi kuwa mapenzi ya Mungu kila mwamini akomae kiroho. Mungu anataka sisi tukue.Neno ya kiyunani lenye maana ya “kukua” lina maanisha “ Kuongezeka,kuwa mwenye kuzaa zaidi au kuwa mkuu”. Wengine tunaposikia kukua kiroho tunaweza kujaribiwa na kufikiri hili jambo linawahusi wa Kristo wachanga walioamini hivi karibuni.Hivyo wao haliwahusu.

Kukua kiroho ni jambo linalomhusika kila mtu aliye mwamini Kristo.Bila kujali lini alifanya hivyo na haya ni mapenzi ya Mungu kwa kila mkristo.Mungu hataki sisi tubakie katika hali ile ile kiroho mwaka hata mwaka. Anatamani kutuona tunabadilika kutoka hatua moja ya utukufu kwenda nyingi mpaka tumegeuzwa katika sura ya Kristo.


Waefeso 4:14

“Ili tusiwe tena watotowachanga, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu...lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie Kristo”.


Mungu anataka kila mwamini awe na tabia ya Kristo.Swali kubwa kwa hiyo ni: Ni kwa namna gani kukua kiroho kunatokea? Tunawezaje kukua ndani ya Kristo?






Maana 7 Za Kukua Kiroho

1. Kukua kiroho ni mchakato wa kufanyika kuwa zaidi kama Yesu Kristo.


Lengo kuu la kukua kiroho ni kuwa kama Yesu. Mpango wa Mungu kwetu sisi tangu mwanzo ni sisi tufanane na Mwanawe. Kukua kiroho ni kubadilishwa kwako kuelekea kufanana na Yesu.

2 Wakorintho 3:18

Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho.

Warumi 8:29

Maana wale aliowajua tangu asili wafananishwe na mfano wa ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.

Tunapoweka imani zetu kwa Yesu,Roho Mtakatifu huanza machakato wa kutufanya kuwa kama Yeye,akitugeuza katika mfano wake.Kukua kiroho penginekunaelezwa vema zaidi katika 2 Peter 1:3-8, ambapo tunaelezwa kwamba kwa Nguvu za Mungu tunacho kila kitu tunachohitaji kuishi maisha ya utauwa ambalo ndio lengo la kukua kwetu kiroho.

Kila tunachohitaji kinatoka kupitia maarifa yetu ya Yeye,ambao ndio ufunguo wa kupata kila tunacho hitaji.Maarifa ya kumjua yanakuja kutoka kwenye Neno tulilopewa kwaajili ya kujengewa na kukua kwetu.


2. Kukua kiroho ni kuongezeka kwa tunda la Roho katika maisha yetu.


Kukua kiroho ni upanuzi wa kutegemea kwako katika kuenenda katika Roho.Kukua kiroho kunaainishwa na Tunda la Roho linavyo ongezeka na kuwa dhahiri katika maisha yetu.

Katika Wagalatia 5:19-23 kuona orodha mbili hapo.Mstari wa 19-21 kuna orodha ya “matendo ya mwili”.Haya ni mambo ambayo yalitambulisha maisha yetu kabla hatujaja kwa Kristo kwa Wokovu. Matendo ya mwili ni mambo ambayo tunaya ungamana na kuyatubu na kwa msaada wa Mungu tunayashinda.

Kadiri tunavyopata uzoefu wa kukua kiroho,ndivyo matendo ya mwili machache zaidi yatajionyesha katika maisha yetu.Kwa lugha nyingine ni kwamba kadiri tunavyi kua kiroho ndiyo matendo ya mwili yanavyi zidi kupotea katika maisha yetu.

Orodha ya pili ni ya Tunda la Roho hii ni mstari wa 22-23.Haya ni matendo ambayo yanapaswa kuwa ni tabia katika maisha yetu baada ya kuwa tunapata wokovu katika Kristo.Kadiri tunavyozidi kukua ndivyo nayo yanavyozikuwa dhahiri katika maisha yetu. 

3.Kukua kiroho ni kazi ya Mungu inayoendelea katika maisha ya muumini baada ya wokovu.

Kukua kiroho ni mwendelezo wa kilichofanyika katika wokovu, wakati maisha mapya yanapotolewa kwa muumini na kuwekwa ndani ya muumini.Kuna pande mbalimbali za ukuaji wetu. Roho Mtakatifu anatuhuisha ili kwamba tuweze kubadilishwa katika sura ya Mungu. Lakini mabadiliko haya ni hatua inayoendelea, na hatua hii inasonga mbele kwa ushirikiano wa Mungu na Mkristo.

Tumeambiwa katika


Wafilipi 2:12-13,

“utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka, kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yangu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.”



Hapa tunaona ushirika ambao ni lazima tufanye na Mungu. Hatuwezi kukaa tu bila kufanya kitu na kufikiri kwamba Mungu peke ataweka ndani yetu kumfanana kwetu. Lazima na sisi tujihusishe vilevile. Ni lazima “tufanye kazi.” Lakini kazi hii siyo ya kutufanya tukubalike na Mungu; isipokuwa ni kuonyesha kuelewa kwetu na kuonyesha shukurani ya msamaha wa dhambi zetu kupitia damu ya Yesu Kristo na kurithiwa kama watoto wa Mungu.


 4. Kukua kiroho ni hali ya mabadiliko ya wokovu kuchukua nafasi ndani yako.

Kukua kiroho ni hatua ya kuuvua utu wa kale na kuuvaa utu mpya.Wengine wanatazama kukua kiroho kama hatua ya kubadilisha utu wa kale wa dhambi kwa utu upya unaotokana na Kristo. Kadiri mtu wa kale anapokufa, mtu mpya anatokea. Wakati hii inapotokea, mtu anakua kiroho.

Pale mabadiliko ya wokovu yanapochukua nafasi ndani ya mwamini,kukkua kiroho huanza.Roho Mtakatifu hufanya makao ndani yetu.(Yohana 14:16-17). Sisi tu viumbe vipya ndani ya Kristo. Utu wetu wa kale wa dhambi unaanza kuacha njia kwaaji ya utu mpya ,Wenye asili ya Kristo.( 2 Kor.5:17, Warumi 6-7).Kukua kiroho ni mchakato mrefu wa maisha yote ambao unategeme na vile tunajifunza na kulitendea kazi Neno la Mungu na kutembea kwetu katika Roho.( 2 Timothy 3:16-17).


5. Kukua kiroho ni kukua katika ufahamu wa kumjua Mungu
Kumjua Mungu ndiyo kusudi na maana ya uzima wa milele. Kisa hasa cha kutaka maisha ya kikristo inatakiwa iwe kumjua Mungu katika kweli. Kwa hiyo, tunapoendelea kukua kumjua yeye katika ukuu wake wote, tunakua kuwa kama yeye.
Nafasi ya kwanza ya utaratibu wa ukuaji inahusisha kukua katika mwanga wa Mungu. Katika Yohana 17:3 Yesu anasema, “Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo aliyetumwa.”

Kadiri tunavyokua katika kumjua Mungu, ndivyo tunavyobadilishwa zaidi na zaidi kuwa katika mfano wake.Ufunguo wa kumjua Mungu ni kuelewa tabia yake ya utakatifu. Tunajifunza kuhisi kama mtume Paulo alivyosema, “Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu” (Wafilipi 3:8a). Hii ni sehemu ya hatua ya utakaso.

Tunapokuwa tunakua katika mwanga wa Mungu katika ukamilifu wake wote, tunakua na kujitambua wenyewe pia. Kipekee, tunafikia kujua hali yetu ya dhambi tofauti na tabia kamilifu ya Mungu. Kadiri tunavyomsogelea karibu Mungu, ndivyo tunavyojiona kuwa mbali naye. Kadiri tunavyomjua alivyo mtukufu kweli, ndivyo kadiri dhambi zetu zinavyodhihirika mbaya zaidi kwetu.


Yeremia 9:23-24

“Bwana asema hivi, mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake, bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifamu mimi na kunijua ya kwamba mimi ni Bwana, nitendaye wema na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo , asema Bwana”


6. Kukua kiroho ni mchakato wa kufanyika kuwa Mwanafunzi wa Yesu.

Biblia inatufundisha kwamba Waamini waliokomaa ndio wanaoitwa wanafunzi.Hili ni Neno ambalo Biblia linatumia kwa waamini waliokomaa tu.Mtu hawezi kuwa mwanafunzi bila ya kuwa chini ya nidhamu.Maneno mwanafunzi na nidhamu yana kwenda pamoja .Disciple – discipline.kadiri ninavyo kuwa nimetiwa nidhamu ndivyo nitavyotumiwa zaidi na Mungu.

Alama ya uanafunzi ni kubeba Msalaba.Mungu anatutaka sisi kubeba Misalaba yetu.Luke 14:27, Luke 9:23.Msalaba huo unabebwa kila siku na kumfuata kila siku.Kubeba msalaba kuna husisha kufanya chochote kila ambacho kitamfanya Kristo kuwa na nafasi ya kwanza katika maisha yangu.


7. Kukua kiroho ni kukua katika Utakatifu wake.


Baada ya kumjua Kristo kama mwokozi, tunatakiwa tuendelee kukua katika mwanga wetu wa utakatifu wa Mungu na katika utambuzi wa hali zetu za dhambi. Hii inaweza kuwa uzoefu wa kuhofisha.
Kumjua Mungu na Utakatifu wake ni kukaribisha kujiweka wazi wenyewe, na huu ni uzoefu wa kutisha kwa hao wanaopenda kuficha makosa yao na mapungufu. Kwa jinsi hiyo, kwa mkristo anayekua, pengo linaonyesha hitaji la kuendelea kumhitaji Kristo na ukuu wa yale aliyofanya msalabani

Kadiri tunavyomjua Mungu ndivyo kadiri tunavyojiona kutofaa mbele zake. Mwanga huu unapokua,tunaona maana ya msamaha wetu na upatanisho wetu kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.

Tunapoufahamu ukuu wa Mungu, (kama Isaya alivyofanya alipoona utukufu wa Mungu hekaluni, au kama taifa la Israeli walivyofanya walipokutana na Mungu katika mlima Sinai). Tunagundua utukufu wa kweli wa mwokozi. Damu yake inaosha wenye dhambi na kuzisafisha na kutuvalisha mavazi meupe ili kwamba tuweze kumsogelea Mungu huyu wa utukufu.


Pastor Meinrald Mtitu.

3 comments:

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...