Sunday, September 24, 2017

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI



Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu

Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtoleaje ?Kila mmoja anaweza kujifunza kutoa,lakini pia inahitaji nidhamu kuwa mtoaji.Hapa ni kanuni 21 za vile tunaweza kumtolea Mungu na hivi ndivyo utoaji wetu unavyopaswa kuwa.



1. TOA KWA UPENDO:

Upendo unapasa kuwa ndiyo kisababisho kikuu nyuma ya kutoa kwetu. Upendo unapaswa kuwa ndio Nia nyuma ya kutoa kwetu.Sio lazima tuoe kwasababu fulani,upendo hautafuti sababu ya kufaidika katika kutoa huko.Tunapotoa kwa upendo si lazima tutoe ili sisi kufaidika. Ukitaka kutoa basi toa bila uchoyo.

“ Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia” Waebrania 6:10


2. TOA KWA KUABUDU ;

Kuabudu ni tendo lolote lile linalo mpa Mungu utukufu, (I Wakoritho 10:31).Kutoa ni sehemu ya Ibada. Askofu David Oyedepo anashauri hivi ,“Toa kama sehemu yako ya Ibada kwa Mungu. Tunatoa kama kuabudu hivyo hatutoi ili kupokea,lakini uaminifu wake Mungu huturudishia Baraka kwetu.”

Hatutoi kama kucheza kamali,Sadaka sio toa na kupokea. “cash and carry”.Ikiwa unatoa tu kwaajili ya kupokea utaaishi kuvunjika moyo na hutaziona Baraka.Toa kama sehemu ya kuabudu.

Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu, Tetemekeni mbele zake, nchi yote.” Zaburi 96:8-9

3. TOA MARA KWA MARA

Kutoa iwe ni sehemu ya maisha yako,hivyo toa mara kwa mara,kila wiki,kila mwezi n.k.Kutoa ni tabia unayoweza kujifunza ni matokeo ya kitendo unachokifanya mara kwa mara.Kadiri tunavyopata nafasi au fursa tuzitumie kuwatendea mema watu wengine.Tafuta fursa za kutoa.Ukizitafuta zitaanza kujitokeza.

“Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho. Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.”-Wagalatia 6:9-10

4. TOA KWA KUMHESHIMU MUNGU:

Kutoa ni ni njia moja wapo ya kumheshimu Mungu.Ni kuonyesha heshima mbele zako,unatambua yeye ni nani na nini anafanya katika maisha yako. “Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.” Mithali 3:9-10,

5. TOA KWA KUKUSUDIA

Toa vile unavyokusudia moyoni mwako au vile unavyoguswa na Kusukumwa.Usitoe kiholela bila kusudi.Huwezi kutoa kwa kila jambo tu,tafuta kusudi la kutoa kwako. Unataka kutoa kwaajili ya kusudi gani?,jambo gani,?eneo gani?,kwaajili ya nini? Tunatoa kwa uangalifu na kwa kupanga katika maombi.Panga kabla kusudi kabla ya kutoa.Panda mbegu yako katika udongo mzuri,usitupe tu mbegu zako hovyo.

“Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.” 2Wakorintho 9:7


6. TOA KWA MOYO WA FURAHA

Kutoa kunapaswa kuwa ni tendo la furaha.Usitoe kwa moyo wa huzuni bali kwa kufuraha.Hisia zako katika kutoa ziwe chanya.Kutoa hakupaswi kuwa na hisia ya maumivu au majuto kwa baada ya kutoa. “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu” 2 Wakoritho.9:7


7. TOA KWA UKARIMU

Ukarimu ni kwa kujali wengine. Ukarimu ni hali ya kujali mahitaji ya watu wengine.Mtu mkarimu anatoa kwa mguso wa ndani,(2 Wakorintho.9:6,13;).Unapotoa kwa ukarimu ni kama unatawanywa,lakini ndivyo unavyoongezewa.” . MTIHALI 11 :24-25
TOA KWA NEEMA YAKE MUNGU.

Utoaji unapaswa kuwa ni matokeo ya kazi ya neema yake Mungu katika maisha yetu,kunaanza kwanza kujitoa kwa maisha yetu yote kwake ,na utoaji ni kama kujazilizia kujitoa kwetu. (2 Kor. 8:1-2,6-7, 9:9-11

2. TOA KWA IMANI

Toa kwa imani ukijua Yeye ameahidi kutupa mahitaji yetu yote,hatutapungukiwa kwa kutoa kwetu,hatutakuwa wahitaji kwasababu tumetoa ( 2 Wakor. 9:7. Wafili 4:19) WAEBRANIA 11:6

3. TOA KI- KIBINAFSI.

Unapotoa toa kama wewe binafsi.Linapokuja suala na utoaji Sio lazima tusuburi utoaji wa pamoja wa kundi au watu wengine.Kutoa kwenye tija katika ufalme wa Mungu ni kule ambako kunasukumwa toka ndani ya kibinafsi.Sio lazima tusubiri mtangazo ndipo tutoe.

( I Wakoritho 16:2)

4. TOA KWA MFUMO

Katika utoaji unayo nafasi ya kujiwekea mfumo wako ambao utautumia katika kumtolea Mungu.Hivyo toa kwa mfumo uliochagua na kujiwekea.Unaweza kuwa na mfumo wa kutenga na weka akiba ya kiasi ambacho unataka kutoa kwaajili ya Bwana ili kisitumike kwaajili ya kusudi jingine.( I Kor 16:2)

5. TOA KWA KADIRI NA UWIANO:

Toa kwa kadiri na uwiano wa ulivyofanikishwa.Katika Agano Jipya tunatoa zaidi kwa kufuata kanuni ya Neema na hiari,kwa kukusudia na kwa kadiri ya vile ulivyofanikishwa.Kadiri unavyokuwa na vingi zaidi toa zaidi.

2 KOR.8:14 Kumbu 16:17, Matendo 11:28-30 I Kor. 16:2,2 Kor:8:3,12, Marko 12:41-44,


6. TOA KUTOKA KATIKA UWINGI.

Toa toka katika uwingi wa vile ulivyo navyo..Kadiri unavyo kuwa na vingi ndivyo unavyotarajiwa kutoa zaidi.

Kumb 28:47,2 Wakor. 9:7


7. TOA KWA HIARI:

Toa kwa hiari yako na kutaka kwako mwenyewe.Maamuzi ya kutoa yaye ni ya kwako mwenyewe,toa kwa kupenda toka ndani.Toa kwa utashi wako mwenyewe ukijua unachofanya,maamuzi ya kutoa yatoke ndani yako.Usitoe kwa msisimko,kwa kufauta mkumbo au kuiga. Toa kwa hiari.( I Nyakati 29:6 Kutoka 25 :2 2 Kor.9:7)

8. TOA KWA UHURU

Toa kwa uhuru bila ya kushinikizwa kutoka nje, Usitoe kwa kufanyiwa hila,kulazimishwa,kutishiwa.

Mtihali 11:24 Warumi 11:35

9. TOA KWA UNYENYEKEVU:

Kutoa kunaanza ni hali nzuri ya ndani yako.Toa kwa unyenyekevu si kwa majivuno,kiburi au kujionyesha.Kabla ya Mungu hajaangalia sadaka yako anakuangalia wewe. MIKA 6:8 MATH.6:2-4


10. TOA KWA NIA NJEMA.

Toa kwa nia njema na na sio kwa hila ,sio kwa sababu au agenda ya siri .Nia yako ya kutoa lazima iwe ni ukarimu,upendo,kumwabudu Mungu n.k.Kutoa kwa nia ya kupokea ni kama kucheza kamali.Mungu hachezi kamali.Ezekiel 33:31, Mathayo 6:33


11. TOA KWA KUWAJIBIKA

Toa kama wajibu wako kama Mkristo.Unapotoa unatimiza wajibu wako wa kiroho. Nehemia 10:34-39 Luka 16:1,2,10

12. TOA KWA KUJIKANA

Toa kwa kujikana nafsi, unabakiwa na kiasi gani baada ya kutoa ndiko kunaonyesha ulijikana kwa umbali gani. Kujitoa kwa kujikana,Daudi alikuwa na Mtazamo huu katika kutoa kwake)hatupaswi kumtolea Mungu wetu mabaki,au makombo,tumtolee kilicho bora na kizuri.Angalia karipio la Nabii Malaki.Mtume paulo anatutaka Kila mmoja wetu anahitaji atathimini upya utoaji wake.( 2 Wakoritho 2:8 Marko 12:41-44, Malaki 1:12-14 2 Samuel 24:24)

13. TOA KWA SIRI

Pale inavyowezekana toa kwa siri.Sio mara zote lazima watu wajue ulivyotoa.Unaweza toa kwa siri na Mungu akakubariki. kutoa kuwe ni kwa usiri pale inapowezekana.Kutoa si mashindano ,kila mtu anatoa kwa kadiri ya neema na alivyojaliwa.( Mithali 21:14, Mathayo 6:2-4)

14. TOA KWA KWA SHUKURANI :

Utoaji ni sehemu yako ya ibada ya shukurani kwa Mungu.Toa kama sehumu ya shukurani kwa Mungu kwa mambo mengi mno aliyekutendea.(I Nyakati 29:9, 2 Wakoritho 9:11)

15. TOA KWA UHURU

Toa kwa uhuru bila ya kushinikizwa kutoka nje, Usitoe kwa kufanyiwa hila,kulazimishwa,kutishiwa.

Mtihali 11:24 Warumi 11:35

16. TOA KWA UNYENYEKEVU:

Kutoa kunaanza ni hali nzuri ya ndani yako.Toa kwa unyenyekevu si kwa majivuno,kiburi au kujionyesha.Kabla ya Mungu hajaangalia sadaka yako anakuangalia wewe. MIKA 6:8 MATH.6:2-4

17. TOA KWA NIA NJEMA.

Toa kwa nia njema na na sio kwa hila ,sio kwa sababu au agenda ya siri .Nia yako ya kutoa lazima iwe ni ukarimu,upendo,kumwabudu Mungu n.k.Kutoa kwa nia ya kupokea ni kama kucheza kamali.Mungu hachezi kamali.Ezekiel 33:31, Mathayo 6:33

18. TOA KWA KUWAJIBIKA

Toa kama wajibu wako kama Mkristo.Unapotoa unatimiza wajibu wako wa kiroho. Nehemia 10:34-39 Luka 16:1,2,10

19. TOA KWA KUJIKANA

Toa kwa kujikana nafsi, unabakiwa na kiasi gani baada ya kutoa ndiko kunaonyesha ulijikana kwa umbali gani. Kujitoa kwa kujikana,Daudi alikuwa na Mtazamo huu katika kutoa kwake)hatupaswi kumtolea Mungu wetu mabaki,au makombo,tumtolee kilicho bora na kizuri.Angalia karipio la Nabii Malaki.Mtume paulo anatutaka Kila mmoja wetu anahitaji atathimini upya utoaji wake.( 2 Wakoritho 2:8 Marko 12:41-44, Malaki 1:12-14 2 Samuel 24:24)

20. TOA KWA SIRI

Pale inavyowezekana toa kwa siri.Sio mara zote lazima watu wajue ulivyotoa.Unaweza toa kwa siri na Mungu akakubariki. kutoa kuwe ni kwa usiri pale inapowezekana.Kutoa si mashindano ,kila mtu anatoa kwa kadiri ya neema na alivyojaliwa.( Mithali 21:14, Mathayo 6:2-4)

21. TOA KWA KWA SHUKURANI :

Utoaji ni sehemu yako ya ibada ya shukurani kwa Mungu.Toa kama sehumu ya shukurani kwa Mungu kwa mambo mengi mno aliyekutendea.(I Nyakati 29:9, 2 Wakoritho 9:11)

Mwalimu Meinrald Mtitu

Light of Hope Teaching Ministries.


1 comment:


  1. WELCOME TO THE GREAT BROTHERHOOD.
    Do you want to be a member of Illuminati as a brotherhood
    that will make you rich and famous in the world and have
    power to control people in the high place in the worldwide
    .Are you a business man or woman,artist, political,
    musician, student, do you want to be rich, famous, powerful
    in life, join the Illuminati brotherhood cult today and get
    instant rich sum of. 2 million dollars in a week, and a free
    home.any where you choose to live in this world
    BENEFITS GIVEN TO NEW MEMBERS of ILLUMINATI.
    1. A Cash Reward of USD $500,000 USD
    2. A New Sleek Dream CAR valued at USD $300,000 USD
    3.A Dream House bought in the country of your own choice
    4. One Month holiday (fully paid) to your dream tourist
    destination.
    5.One year Golf Membership package
    6.A V.I.P treatment in all Airports in the World 7.A total
    Lifestyle change 8.Access to Bohemian Grove
    account every month as a member
    9.One Month booked Appointment with Top 5 world
    Leaders and Top 5 Celebrities in the World.
    If you are interested of joining us in the great brotherhood of illuminati CONTACT MR ROLAND or WhatsApp him +2348142587627
    or email:illuminatipower666brotherhood@gmail.com

    ReplyDelete

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...