Kiongozi Mtumishi

Mathayo 20:25-28
Lakini
Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu,
na wakubwa wao huwatumikisha. Lakini haitakuwa hivyo
kwenu; bali mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu; na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe
mtumwa wenu; kama vile Mwana wa
Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya
wengi.
Wafuasi
wa kwanza wa Yesu walidhania kwamba uongozi unamaanisha Nguvu,nafasi ya heshima
na utukufu.Na siku moja wawili miongoni mwao wakaomba nafasi ya mamlaka mmoja
kuwa upande wa kushoto na mwingine wa kulia.
1. Ukubwa sio kuwa juu ya wengine bali kuwatumikia wengine.
Yesu
Kristo ni mfano wa kuuigwa wa Kiongozi Mtumishi ambaye amewahi
kuishi hapa duniani Yeye alitumia tukio kufafanua na kuweza wazi kwa
wanafunzi wake wote ni maana ya Ukubwa. Maana ya ukubwa kwa mujibu wa
Yesu ni si kuwa bwana juu ya wengine bali kuwatumikia wengine. “Kwa maana Mwana wa Adamu
naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.” (Marko 10:45)
Rick
Warren anasema, “Wanafunzi wa Yesu walishindania juu ya nani atachukua
nafasi ya juu, na miaka 2,000 badaye, viongozi wa Kikristo
bado wanapigania nafasi na kujulikana katika kanisa,madhehebu na huduma shiriki
za kanisa.”
Uongozi
wa kiutumishi ni muhimu leo kwasababu kutokuwa na matumaini kuna kuongezeka kwa
kasi kupita kupatika kwa masaada.Watu wanahitaji kuwaamini na
kuwategemea viongozi na katika kanuni zinazofanya kazi.
2. Uongozi ni jukumu la kuwatumikia wengine

Vile
ulimwengu unavyosema kuhusu kiongozi halisi ni yupi ni toafauti kabisa na vile
Yesu alivyosema.
Yesu anasema kwamba kuwa
kiongozi sio suala la kuwafanya watu wakutumikie,bali uongozi ni suala la
kuwatumikiwa wao.Kadiri ninavyo watumiki wengine zaidi,ndivyo Mungu
anavyoniinua zaidi katika utumishi.Yesu anasema kama unataka kuwa Mkubwa wa
wote,ni lazima ujifunze kwanza kuwa mtumishi wa wote.
MATHAYO 20:26-28
Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu ye
yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu; na mtu
ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu; kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali
kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.

LUKA 22:24-27
Yakatokea mashindano kati
yao, kwamba ni nani anayehesabiwa kuwa mkubwa. Akawaambia, Wafalme wa Mataifa huwatawala, na wenye
mamlaka juu yao huitwa Wenye fadhili; lakini
kwenu ninyi sivyo; bali aliye mkubwa kwenu na awe kama aliye mdogo; na mwenye
kuongoza kama yule atumikaye. Maana
aliye mkubwa ni yupi? Yeye aketiye chakulani, au yule atumikaye? Siye yule
aketiye chakulani? Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye.
3. Kutisha na kutawala wengine kwa nguvu sio Utumishi.

4. Moyo wa utumishi ndio msingi wa uongozi

Leo
utumishi umepoteza maana yake ,Mtumishi wa leo ni bosi,ni mtu wa kunyenyekewa,
anaye lindwa na walinzi maalumu waliovalia makoti marefu na miwani mieusi,Yesu
hakuwa na mlinzi hata petro alipojitolea alimvunja moyo
kumlinda.Watumishi wa leo ni kujipa majina makubwa makubwa,kujigamba sana
,kujisifu kupita kiasi, kushindanisha utajiri walio nao n.k. Huu sio utumishi alio ufundisha Bwana Yesu.
Meinrald Mtitu.
No comments:
Post a Comment