Tuesday, August 8, 2017

ZIJUE DHORUBA ZA MAISHA



Dhoruba Ni Njia Ya Mungu Kukujaribu Na Kuithibitisha Imani Yako


Mathayo 14:25-31

Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? 

Wakati Yesu anawajia akitembea katika maji,wanafunzi hawakuweza kumtambua.Walifikiri ni pepo au kivuli chake.Wakapiga kelele kwa hofu.Lakini Yesu alikuja na ujumbe wa amani na wa nguvu.Alikuwa na ujumbe wa Amani kwao.

Dhoruba za maisha zina uwezo wa kumfunua Mwokozi kwetu katika njia ambayo hatu kuzingatia kabla.Anapokuja kwetu,akitembea katika dhoruba zetu,hutupa ujumbe ule ule wa matumaini ambao waliwapa wanafunzi usiku ule.

Walikuwa bado wapo kwenye dhoruba pale alipo waambia wachangamke.Kwa uweza wake,Mwana wa Mungu anaweza kutupa amani katikati ya dhoruba zetu. Hii ni amani anayoitaja katika Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. 

Yesu alipojitokeza,alitokea akisema juu ya utambulisho wake, ”Ndimi”. “Mimi Ndiye”.Ni kauri kama ile aliyoisema kwamba Mimi Ndimi mlango,Mimi Ndimi njia ,kweli na Uzima,Mimi Ndimi mzabibu wa kweli,Mimi Ndimi mchugnaji mwema.

Yesu anawaambia wanafunzi wake wa furahi, Mungu yupo hapo.Tukiweza kuukamata ukweli kwamba Yesu ni Ndimi Mkuu na kwamba ana nguvu zote mbingu na dunia sawa na Mathayo 28:18,tunaweza kufarahia amani katikati ya majaribu.

Yesu analitoa ujumbe wa uwezo,alitioa amri kwa wanafunzi wake wasiogope.Tukiweza kuona ukweli kwamba Yesu anatawala kila eneo la maisha yetu,na kwamba ni Mungu ,na kwamba anazo nguvu zote,basi tunaweza kufika mahali ambapo tunaweza kumtumaini kabisa kupitia dhoruba zote za maisha.

Dhoruba za maisha ni Baraka kwasababu zinamfunua Mwokozi katika namna mpya kabisa.

Mathayo 14: 28-29,

Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. 

Dhoruba zinatutakasa.Pale Petro aliposikia kwamba ni Bwana alitaka kujiunga na Yesu kutembea katika maji.Yesu alimwambia tu Petro njoo.Petro aliitii na yeye akatembea katima maji.Yesu aliitumia dhoruba kama namana ya kumsaidia Petro kukua katika imani.

Pale dhoruba za maisha zinapotupiga kama tunataweza kuushika ukweli kwamba Yesu ni Bwana wa dhoruba,na sisi pia tunaweza inuka juu ya mazingira yetu na kutembea juu ya mawimbi na pamoja na Bwana.Dhoruba zinaweza kuinua viwango vyetu vya imani katika kumtumainia Bwana.

Natambua fika kwamba kutembea kwa Petro hakukudumu kwa muda mrefu.Punde alipoondoa macho yake kwa Bwana alianza kuzama.Hata hivyo,Petro ameacha ushuhuda ambao wanafunzi wengine hawakuwa nao.Ni yeye pekee anayeweza kusema niliwahi kutembea juu ya mawimbi.

Hakika Mungu anaweza kuzitumia siku zetu ngumu kutufundisha zaidi kumhusu Yeye na kutusaidai kukua katika Bwana.Atatumia mawimbi kukufanya uwe zaidi kama yeye.Kumbuka kulikuwa na watu kumi na mbili kwenywe mtumbwi lakini ni mmoja tu anayeweza kusema alitembea katika dhoruba kama Yesu.

Dhoruba Za Maisha Zinatukumbusha Ni Nani Ambaye Anatawala.

Mathayo 14: 30-31 

Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?

Petro alipotaka kutembea juu ya maji kama Yesu,Alimjaribu Bwana na akaingia katika maji.Hata hivyo pale alipotoa macho yake kwa Bwana na alipofanya hivyo alijikuta mwenywe kwenye matatizo. Lakini mara moja alikumbuka nani ambaye anatawala na akamwita Bwana na akapata masaada alio uhitaji.

Dhoruba za maisha zinatumika kutukumbusha sisi juu ya nani anayetawala.Kama Petro,kuna wakati tunaondoa macho yetu kwa Bwana wakati wa dhoruba zetu.Tunapofanya hivyo,tunajihakikishia kufeli au kushindwa.Tunahitaji kukumbuka nani ni msimamizi wa kila kitu.

Kama tutashinda na kufauli kwenye dhoruba za maisha hatustahili sifa kwamba ni kwa uwezo wetu au mafanikio yetu.Bali ni kwasababu kuna mmoja aliye mkuu kuliko sisi anaye tushika mkono. Mafanikio yetu na ushindi katika dhoruba za maisha yapo juu ya utayari wetu wa kutambua kwamba Yesu ni Bwana juu ya dhoruba.

1 comment:


  1. WELCOME TO THE GREAT BROTHERHOOD.
    Do you want to be a member of Illuminati as a brotherhood
    that will make you rich and famous in the world and have
    power to control people in the high place in the worldwide
    .Are you a business man or woman,artist, political,
    musician, student, do you want to be rich, famous, powerful
    in life, join the Illuminati brotherhood cult today and get
    instant rich sum of. 2 million dollars in a week, and a free
    home.any where you choose to live in this world
    BENEFITS GIVEN TO NEW MEMBERS of ILLUMINATI.
    1. A Cash Reward of USD $500,000 USD
    2. A New Sleek Dream CAR valued at USD $300,000 USD
    3.A Dream House bought in the country of your own choice
    4. One Month holiday (fully paid) to your dream tourist
    destination.
    5.One year Golf Membership package
    6.A V.I.P treatment in all Airports in the World 7.A total
    Lifestyle change 8.Access to Bohemian Grove
    account every month as a member
    9.One Month booked Appointment with Top 5 world
    Leaders and Top 5 Celebrities in the World.
    If you are interested of joining us in the great brotherhood of illuminati CONTACT MR ROLAND or WhatsApp him +2348142587627
    or email:illuminatipower666brotherhood@gmail.com

    ReplyDelete

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...