Tuesday, August 8, 2017

KUZISHINDA DHORUBA KATIKA MAISHA YAKO


Pamoja na kuwa dhoruba katika maisha yetu sio nzuri, lakini bado zina tengeneza manufaa fulani katika maisha yetu.Kuna Baraka zilizojificha katika dhoruba za maisha zinazo tupiga sisi kama wana wa Mungu.Sijui ni aina gani ya dhoruba unayokabiliana ,lakini ninajua kwamba Bwana analo kusudi katika kuiruhusu dhoruba na tufani ipige katika maisha yako.


Mathayo 14:22,24

Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng'ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano. Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho.

Katika kifungu hiki cha maandiko,tunaona vile wanafunzi wa Bwana wakiwa wamekwama katika dhoruba kali.Walijikuta katika dhoruba ile,kwasababu walikuwa wameamriwa na Bwana kuvuka bahari ya Galilaya.Watu hawa walikuwa katika mapenzi ya Mungu na bado,wanaonekana wana hangaika katika dhoruba. Pamoja na kujitahidi kote,hata hivyo,inaonekana hawawezi kusonga mbele,Upepo unawapiga usoni .Watu hawa 12 wana kwamba katika dhoruba na washindwa kutoka. 

Je umewahi kujikuta katika hali kama hiyo? Umewahi kujikuta umekwama kwenye moja wapo mwa dhoruba za maisha,na haijalishi kiasi gani umejitahidi kujaribu, inaonekana umeshindwa kwenda mbele? Sawa,sote tuna nyakati kama hizo! Inaonekana kama dhoruba haitaisha na hakuna jema litakalo kuja kutoka kile tunacho kikabili.Hata hivyo pamoja na kuwa dhoruba katika maisha sio nzuri,zina tengeneza faida /manufaa fulani katika maisha yetu.

Dhoruba Ni Njia Ya Mungu Ya Kukujia na Kujifunua katika Maisha Yako. 


Mathayo 14:25-

Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.


Marko 6:48-

Akawaona wakitaabika kwa kuvuta makasia, kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho; hata ilipopata kama zamu ya nne ya usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; akataka kuwapita.


Yesu alikuja katikati ya majanga ya upepo makali na mawambi makali wakati wanafunzi walipokuwa wanapigania kuokoa maisha yao katika dhoruba.Napata picha kwamba hawa watu walikuwa wanaogopa juu ya maisha yao.Wakati walipofikiria kwamba matumaini yote yamekwisha na wamebaki bila matumaini,Upande wa pili Yesu anakuja akitembea katika mawimbi yale yale na upepo ule mkali akiwaendea.

Lile jambo ambalo wanafunzi waliogopa yaani bahari iliyochafuka,ndilo hilo hilo ambalo Mungu alilitumia kama njia cha kujifunua mwenyewe kwao.Atafanya hivyo hivyo katika maisha yako na yangu.Yesu aliwajia usiku bahari wakati wanaogopa.Biblia inasema Yesu aliwajia kwenye zamu ya Nne.Ambayo ni kati ya saa 9 na 12 Asubuhi,ni katika masaa ya giza ya usiku,Yesu alikuja kwao akitembea juu ya maji.

Jambo lile wanafunzi waliloliogopa,bahari iliyochafuka,ndicho kitu kile ambacho Mungu alitumia kuwaendea wao.Huu ni ushuda wa ajabu!Hakuwa anawaambia kwamba dhoruba haikuwa kali,alikuwa anawaambia kwamba alikuwa ni mkuu kuliko dhoruba.Hilo bado ni neno lake kwako! Pamoja na kile unachokikabili katika maisha,kumbuka Yesu ni mkuu kuliko dhoruba unayoweza kuwa unaipitia.

Unaweza kuwa unatembea katika giza na unashanga Yesu yupo wapi.Unaweza kuwa unazikabili siku fulani za giza katika maisha yako hata sasa.Ngoja nikukumbushe kwamba Mungu wetu yupo siku zote pamoja nawe sasa na Neno lake katika Waebrani 13:5 ambapo anasema, “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.” 

Ngoja nikukumbushe kwamba hata katika saa ya giza kabisa ya maisha yako Mungu bado ni Mungu na bado anatawala maisha yako. Hata saa ya giza sana ya maisha haiwezi kukuficha wewe kutoka katika uso wa Mungu.Yeye yupo hapo hata kama huwezi kumwona.


Mungu anaweza asikuzuie kuingika katika dhoruba,lakini atakutunza katikati ya dhoruba.

Kuna nyakati tunajihisi kama tumepoteza vita vyetu na dhoruba zetu,lakini wacha ni kukumbushe kwamba kama vile kwa hakika Bwana anatawala baraka zako.Yeye pia anatawala dhoruba zako.Wakati mambo yanaoneka ni mabaya kabasi,hebu angalia kukuzunguka,Yesu yupo karibu kujionyesha!Kumbuka anaweza asikuzuie kuingika katika dhoruba,lakini atakutunza katikati ya dhoruba.

Fikiria juu ya Vijana watatu wa kiebrania, Fikiri juu ya Danieli na Nuhu.Mungu hakuwazuia yeyote kati yahawa kuuingia katika dhoruba,lakini aliwaokoa wote kutoka katika dhoruba zao.Kile alichofanya kwao,atafanya kwako.

Kama utakuwa na subira na kumngojea, Yeye,atajionyesha katika wakati sahihi.Utaona vile Bwana atavyoitumia dhoruba kujiweka wazi kwako. Yaani kitu kile kile kinachokuogopesha kitakuwa ni chombo ambacho Bwana atakitumia kujionyesha na kujidhihirisha ukuu wake katika maisha yako.

Mungu alitumia dhoruba ya mwiba katika maisha yake Mtume Paulo ili kujionyesha na kujidhihirisha katika maisha ya Paulo.

2 Wakoritho.12:7-10.

Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu. 

Kile ninachojaribu kukuambia ni hiki: “ Usiogope dhoruba katika maisha! Dhoruba imesanifiwa na Bwana kama njia ya kumleta Yeye karibu kwako.Aliyazipanga na zipo kwaajili ya faida yako.”

Warumi 8:28 “ Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.”

Mungu Akubariki.

No comments:

Post a Comment

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...