Wednesday, September 13, 2017

KUBADILISHWA KUPITIA MATESO



KUBADILISHWA KUPITIA MATESO 

Tunapokutana na nguvu za Mungu tukiwa katika mateso tunakuwa kama Ayubu.Maswali yetu yote kwa Mungu, malalamiko yetu yote yanayeyuka na tunaishia kuanguka mbele zake kwa hofu na kumwabudu.Tunakuwa hatuna tena cha kuzungumza mbele zake.
AYUBU 42:1-6

Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema. Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika. Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua. Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie. Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. Kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu, na kutubu Katika mavumbi na majivu.

Baada ya Ayubu kumtaka sana Mungu ajitokeze na amjibu kwanini anamtesa,hatimaye katika sura ya 38-41 Mungua najitokeza kupitia Upepo wa Kisurisuri na kumjibu Ayubu kwa kumuuliza maswali mbalimbali.Hatimaye sasa katika Sura ya 42 Ayubu anasalimu amri anamwelewa Mungu na hana swali tena kuhusu kwanini anateseka.Kile kitendo cha kukutana na uwepo wa Mungu kinabadilisha,mtazamo wake unabadilika,maswali yake yanaisha na kukoma.


Ayubu atanapata uzoefu mpya na anahitimisha kwa kile alichojifunza pale Mungu alipomtokea. Mungu halimjibu Ayubu kwa mahojiano na sio kwa kujibu maswali yake.Mungu alijibu kwa kujitokeza tu kwa uwepo wake.Hilo tu lilitosha kumbadilisha Ayubu.

Nafikiri wakati mwingine tukiwa katika vipindi vya mateso kama Ayubu tunachohitaji zaidi ni uwepo wa Mungu tu ,huuo utamaliza maswali yetu yote.Na kubadilisha matazamo wetu kuhusu mateso tunayoyapitia.

Baada ya Mungu kutokea na Kuhojiana na Ayubu tunanona hata alipopata nafasi ya kuzungumza ,alizungumza kama mtu aliyebadilika kabisa na aliyenyenyekea sana.Hakuendelea tena kuwa na madai ya majibu toka kwa Mungu.Hakuendelea tena kushikiria msimamo wake na kusisitiza kuwa yeye ni mwenye haki hivyo hakusatahili hayo mateso.

Baada ya hapo Ayubu alikuwa kimya.Baada ya maneno yote katika sura za nyuma ,hakuna tena maneno yanayorekodiwa kutoka kwenye kinywa cha Ayubu. Kumwona Mungu,na kuelewa Nguvu za Mungu kulibadilisha kabisa mtazamo wa Ayubu.Aliifanya upya hofu yake ya Mungu na ilikuwa ni hofu nzuri.

Mambo Makuu Matano Yakujifunza Katika Vipindi Vya Mateso

Masomo haya ni ya muhimu,hasa kama kama utakuwa kwenye msimu wa maumivu na kuteseka.Kile Ayubu aligundua kupitia mateso yake miaka mingi iliyopita hata leo kinawapa watu nuru ya ukweli ambao bado haujapoteza nguvu yake.


1. Mungu anaweza kutenda mambo yote.

AYUBU 42;1-2

Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema. Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote.

Ayubu alijifunza juu ya uwezo na ukuu na enzi ya Mungu.Alikiri kwamba hakika Mungu anaweza kutenda mambo yote.Yeye anatawala juu ya vyote.Hili ni somo kubwa sana la kujifunza.Baada ya kupitia katika mateso Imani ya Ayubu ili kuwa imetakaswa na imeimrika zaidi.Aliaamushwa na kuwa na ufahamu Mpya wa Kina kuhusu Mungu na uwepo na ukuu wake.Sasa imani yake imepita katika moto na amekuwa na kumjua Mungu kwa karibu zaidi.

Kumbe katika mateso tunapata nafasi ya kumjua Mungu kwa upya. Kuna kupata ufunuo mpya kupitia mateso ambao usingeweza kuupata kwa njia yeyote ile.


2. Makusudi yake Mungu hayawezi kuzuilika

AYUBU 42 : 2b Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika. 

Jambo jingine ambalo Ayubu alijifunza katika mapito yake ni kuhusu makusudi ya Mungu. Aliyefahamu makusudi ya Mungu na akaukubali ukweli kwamba makusudi ya Mungu hayawezi kuzuilika. Ayubu alijifunza somo kuhusu njia za Mungu kwamba Mungu anakwenda kufanya kile anachoenda kufanya.

Mungu hutuamsha tuujue ukweli kwamba Yeye ni Mungu wa makusudi. Mungu anayo makusudi na maisha yetu na anapokusudia kufanya jambo haiwezekani kwa chochote kile kulizuia hilo kusudi lake.Wakati mwingine ni kupitia hayo mateso tunayatambua makusudi ya Mungu na kujisalimisha kwake.



3. Ufahamu wetu ni mdogo kuelewa Maarifa ya Mungu ya kuruhusu Mateso kwetu. 


Ayubu 42:3

Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua. 

Baada ya kuziona njia za Mungu katika Ukuu na enzi yake Ayubu alikiri kwamba ufahamu ulikuwa ni mdogo sana kuelewa kwanini anateseka. Alitambua kwamba hata kama Mungu angemwelezea kila kitu anachofanya na kumchambulia kimoja kimoja bado asingeweza kuzielewa njia za Mungu kwani ni kuu sana kwa akili yake kuelewa. ( Isaya 55: 8-9). Alijifunza kwamba kuna wakati katika mahusiano na Mungu huitaji kujua kwanini; unahitaji kuwa mtii tu.


4. Maarifa ya Mungu ni makuu sana na ya kushangaza sana.

Ayubu 42:5

Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. 

Mahusiano ya Ayubu na Mungu yalikuja kuwa ni ya kina na ya karibu kwasababu ya yale aliyopitia.Ni kweli kuanzia mwanzo hata kabla ya kupitia mateso alikuwa ni mtumishi mcha Mungu na mwaminifu,lakini sasa anazunguza juu ya ufunuo binafsi alioupata wa kukutana na Mungu uso kwa uso. Kukutana kwake na Mungu kulifanya kila kitu katika maisha yake kubadilika.

Kupitia mateso uhusiano wetu na Mungu unakuwa ni wakaribu na halisi .Hakuna wakati tunakutana na uwepo wa Mungu kwa karibu kama wakati wa mateso. Ni katika nyakati kama hizo ni rahisi zaidi kupata ufunuo wa Kibinafsi kuhusu Mungu.

Wakati Shetani anataka kutumia maumivu yako kukufanya ukwazike na kukosana na Mungu;Mungu anataka kutumia maumivu yako kukuvuta kwake ili aweze kuleta badiliko ndani yako.Kitu kile kile ambacho Shetani anataka kuyatumia mateso kukufanya akuvute mbali na Mungu ,Mungu atatumia mateso haya hayo kufanya wewe kumjua Yeye kwa ukaribu zaidi kuliko Mwanzo.

5. Mateso hutufanya kupondeka na kujishusha mbele za Mungu.

AYUBU 42:6

Kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu, na kutubu Katika mavumbi na majivu. 

Mara nyingi Mungu alipojifunua kwa watu katika Biblia ,huu ulikuwa ndio mwitikio wa kawaida.Ayubu alipotokea na Mungu katika mateso yake alipondeka na kujishusha mbele zake.Kuna hali kuu sana ya kujiona hastahili na mwenye upungufu. Ili hali ya Ayubu aliyokuwa ameing’an’gania ya kujiona ni mwenye haki na hastahili kuteseka ilikwisha.

Mateso yanatunyenyekeza na kutufanya tumtegemee Mungu.

Ayubu alifanya toba kwa maneno yake na mwitikio wake mbaya aliouonyesha katika kipindi chote cha kujaribiwa katika mateso.Tunamwona Ayubu Mpya ambaye amenyenyekea na kupondeka kabisa. Ambaye mbali na nje ya Mungu anatambua kwamba ana haki ya kujihesabia,anayetambua udhaifu wake, upungufu wake, kutokuwa na umuhimu na utupu wake .

Kwasababu ya kutakaswa kwa moto wa mateso Ayubu sasa ametoka akiwa anaweza kutembea katika unyenyekevu mbele za Mungu na kumtegemea Mungu katika maisha yake yote.

Watu wengine Majaribu yana washinda, lakini wengine yana waimarisha inategemea na namana gani tunashughulika nayo.

2 Wakoritho 1:8-10 

Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi. Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu, aliyetuokoa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; ambaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa; 

Mateso na dhiki zilimfundisha Paulo asijitegemee Mwenyewe bali Mungu.Mungu ataendelea kuruhusu mateso ,dhiki, taabu,adha mbalimbali kwa watu wake pale wanapoanza kuwa wanajitegemea wenyewe na kushindwa kumtumainia Yeye.Ni kupitia mateso watu huwa wanaona kwa urahisi umuhimu na uhitaji wa Mungu.


Mwalimu Meinrald Mtitu




No comments:

Post a Comment

KANUNI 21 ZA KIBIBLIA ZA UTOAJI

Kanuni 21 Za Jinsi Ya Kumtolea Mungu Mungu anatutarajia tumtolea katika mali na mapato yetu( Fedha zetu) anayotubariki,lakini tuna mtolea...